Wajumbe wa
Board,
22/5/2017
Special Olympics Tanzania,
S.L.P. 42979,
DAR ES SALAAM.
Ndugu,
YAH: TAARIFA YA UJIO WA RAIS WA SPECIAL OLYMPICS KANDA YA AFRIKA
Rejeeni kichwa cha habari hapo juu.
Napenda kuchukua nafasi hii
kuwapeni taarifa kuwa rais wa chombo chetu cha Special Olympics Kanda
ya Afrika ambaye pia ni mtendaji mkuu Bw. Charles Nyambe anatarajia
kufanya ziara katika Program yetu ya Tanzania kuanzia tarehe 5/6/2017
hadi 9/5/2017.
Akiwa hapa Tanzania atapata fursa
ya kuendesha mafunzo ya uongozi wa michezo ya Special Olympics kwa
makocha 50, (nimeona wawe waratibu wetu wa mikoa yote 30, pamoja na
wengine 20 kutoka Dar es Salaam).
Amependekeza pia kutumia masaa
matatu kati ya siku nne atakazokuwa nasi hapa Tanzania kukutana na
kuendesha mafunzo ya uongozi kwa wajumbe wote wa board ya Special
Olympics Tanzania.
Naomba taarifa hii itumike kama
mwaliko wa kuhudhuria mafunzo tajwa hapo juu katika siku na tarehe
ambayo mtatangaziwa kwa kadri atakavyopendekeza na kupanga yeye
mwenyewe.
Ahsante
Charles Rays
Mkurugenzi Special Olympics Tanzania.
Tags
MICHEZO