![]() |
| Msitahiki Meya Prof Davis Mwamfupe akisisitiza jambo mara baada ya kuchaguliwa kwake, kwenye Baraza maalumu la uchaguzi wa meya |
![]() |
| Msitahiki Meya Prof Davis Mwamfupe akiteta jambo na Mbubunge wa jimbo la Dodoma Mjini Anthon Mavunde nje ya ukumbi wa Mikutano baada ya kuchaguliwa kwake jana July 19,2017 |
![]() |
| Hili Ndilo Pozi za aliyekuwa Kaimu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumanne Ngede Baada ya uchaguzi wa Meya mpya Pfof. Davis Mwamfupe PICHA ZOTE NA JOHN BANDA MMILIKI WA BLOG HII |
![]() |
| Madiwani wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa manispaa wakati Baraza Maalumu la uchaguzi wa meya likiendelea July 9,2019 |
MSTAHIKI MEYA mpya wa Manispaa ya Dodoma PROF. Davis
Mwamfupe amesema imefika wakati ambao
viongozi, wanasiasa na wananchi wote wanatambua kuwa manispaa hiyo haina picha
ya kawaida kama ilivyo kwa manispaa nyingine hapa nchini kwakuwa macho ya ndani
na nje ya nchi yanaiangalia kwakuwa ndipo makao makuu ya nchi yalipo
Akiongea katika mahijiano maalumu na kituo hiki
ofisini kwake mara baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi hiyo na aliyekuwa kaimu
Meya wa manispaa hiyo Jumanne Ngede, Mwamfupe amesema Jukumu alilonalo kwa sasa
ni kuwafanya wakazi wake kutambua hilo
Aidha Meya huyo Msomi ambaye aliwahi kuwa Mshiriki
wa Bunge Maalumu la Katiba na Mkufunzi wa semina mbalimbali za wabunge amesema
anatambua fika kuwa Mameya wawili waliwahi kujiuzuru kutokana na ubadhilifu
akiwemo aliyemtangulia Jaffary Mwanyemba kuwa tabia hiyo ni huruka ya mtu mwenyewe hivyo
linaloweka nidha katika taasisi yoyote ni ushirikishaji na ushirikishwaji katika kila jambo
Awali Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Christina
Mndeme mara baada ya uchaguzi wa meya huyo akamwambia mambo muhimu ya kuanzia
kazi ikiwemo kudhibiti Ubadhirifu katika miradi ya maendeleo, kuondoa Mchwa anaevitafuna vyama vya ushirika na kahakikisha Dawa za Muhimu za Binadamu zinapatikana katika hospitali, vituo vya afya na Zahanati tena kwa bei nafuu.
Tags
Meya Dodoma





