![]() |
Mwarabu aliyedaiwa kuuawa Morogoro akiwapa mikono wakazi wa kata ya kizota waliokusanyika kwa lengo la kuhakikisha kuwa ni kweli yeye |
Na John Banda, Dodoma
kijana mmoja aitwaye Seif Ramadhan Mwarabu umri 29 kuibuka
akiwa hai siku nne tangu kufanyika kwa mazishi yake baada ya uliodaiwa kuwa ni mwili wake kuokotwa maeneo ya Msamvu
Mkoani Morogoro na kusafirishwa na ndugu zake mpaka Dodoma kwa mazishi.
BLOG hii ilipiga hodi maeneo ya Kizota hapa Mjini Dodoma kwa lengo la
kuzungumza na ndugu zake ili kupata
ukweli na kuthibitisha kinachosemwa.
Kwanza
Mjomba wake Iddi Salum ambaye alitumwa na familia yake kwenda Morogoro
kuutambua mwili wa marehemu na kuurudisha nyumbani kwa taratibu za mzishi.
Naye mama yake mzazi Bi Sarah Michael akizungumzia jambo hili
ambalo linaleta mashaka na kuacha maswali mengi amesema baada ya mwili kufika
kutoka Morogoro aliukagua na kuthibitisha kwamba ni wa mtoto wake lakini
alishangaa siku tatu mbele kupokea simu kutoka Dar es salaam kwa mtoto wake huyo akisema kuwa yumzima wa
afya.
Aidha nimezungumza na Seif mwenyewe akisema anashangazwa na
taarifa hizo za kifo chake ilihali yeye ni mzima.
Hata hivyo bado wengi wanajiuliza mkasa mzima wa kijana Seif
ikionekana kama ni maigizo kwani ni siku kadhaa tu zilizopita walishiriki mazishi
yake , lakini sasa wanashangazwa kumuona akiwa mzima kiasi kwamba watu wanamiminika
nyumbani kwao kutaka kumuona na kujiridhisha kama kweli ni yeye.
Hata
hivyo kumesomwa Duwa ya kumuombe uhai mrefu kijana Seif iliyoongozwa na
shekh wa msikiti wa Kizota Ahmad Suleiman Mkoma ambapo baada ya Duwa
hiyo aliwataka ndugu Kumchukulia Marehemu aliyeokotwa mkoani Morogoro na
kuzikwa Dodoma kwa jina la Seif Ramadhan Mwarabu kuwa ndugu yao na
hivyo kulitunza kaburi lake.
Tags
kIZUNGUMKUTI










