BANDA MEDIA BLOG

‘THIS IS SIMBA’HAIJAWAHI KUTOKEA,YADUNGUA RAYON SPORTS YA RWANDA


IMG_9502
Simba imeishinda Rayon Sports kwa bao 1-0 katika mechi nzuri ya kirafiki iliyokuwa maalum kwa ajili ya tamasha la Simba Day.
Tamasha hilo ambalo hufanyika kila Agosti 8 ya kila mwaka lilifana kwa mambo mbalimbali ikiwemo kutambulishwa kwa wachezaji wapya wa Simba.
IMG_5164-1
Simba walianza kupata bao dakika ya 24 likifungwa na kiungo hatari kwa sasa Ibrahimu Mohamed ‘MO’ aliyepokea pasi safi kutoka kwa Emmanuel Okwi na kuwa chambua mabeki wa Rayon ambayo iliweza kuwaacha wachezaji sita muhimu ambao wapo kwenye timu ya Taifa ya Rwanda inayojiandaa naa Chan dhidi ya Uganda.
niyo
Hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao hilo moja na kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko Simba ikimuingiza kiungo wao hatari Haruna Niyonzima kipenzi cha wana Yanga aliyehamia Msimbazi na alionesha uhodari mwingi kwa kuuchezea Mpira kwa madaha.
IMG_5204
Kama Simbaa wangekuwa makini wangeweza kutoka na ushindi mnono kwani mshambuliaji wao hatari John Bocco aliweza kukosa nafasi mbili za wazi akiwa yeye na golikipa hadi mpira uanaisha Simba wameibuka na ushindi wa bao 1-0 na kusherekea vizuri siku yao ya Simba Day ambayo imetimiza miaka tisa tangu kuanzzishwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG