
Kwa vyovyote vile, hivi sasa bado ni mapema sana kujua ni nani hasa wahusika wa tukio hili la kinyama na dhamiri yao, lakini, kwa niaba yetu na wanachama wetu, mawakili wa Tanganyika, tunalaani na kukemea vikali kitendo hiki cha kihalifu na cha uoga mkubwa.
Wito wetu kwa vyombo vya ulinzi na usalama ni kwamba wafanye kazi yao kwa umakini, haki na weledi ili kuwapata watu waliofanya unyama huu na kuwafikisha katika vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake. Sisi kwa upande wetu tunalifuatilia suala hili kwa ukaribu, na tutaendelea kuufahamisha umma kinachoendelea.
Mwisho, tunatoa pole kwa familia ya Mh. Tundu Lissu, ndugu na jamaa zake, wanachama wetu wa Chama cha Mawakili Tanganyika na watanzania wote ambao wameguswa na tukio hilo. Tunaomba kila mmoja wetu kwa imani yake amuombee ndugu yetu Mh Tundu Lissu apone na apate nafuu haraka ili tuungane naye tena katika shughuli zetu za kila siku.
Tunawaomba wanachama na watanzania wote waendelee kuwa wavumilivu na watulivu wakati huu. Na kuujumla wetu tulaani na kukemea kitendo hiki ambacho hakikubaliki katika mila na desturi zetu kama Taifa.
Ahsanteni.
Imetolewa na
Godwin Simba Ngwilimi (Wakili), Makamu wa Rais, TLS,
Kwa niaba ya Baraza la Uongozi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)
Dar es Salaam
Tags
Tundu Lisu