![]() |
| Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Gilles Muroto akiwaonyesha waandishi wa habari hawapo pichani sale za Jeshi la Wananchi zilizokuwa zikitumika kinyume na utaratibu |
| Gari alolikua akitumia Tundu Lisu likiwa pamoja na magari mengine nje ya ofisi za Polisi Mkoa wa Dodoma |
Na JOHN BANDA
-DODOMA
JESHI la Polisi Mkoa wa
Dodoma limesema bado linaendelea kumtafuta dereva wa Tundu Lissu,Simon Bakari Mohammed
huku likimtaka popote alipo ajisalimishe katika Kituo chochote cha Polisi.
Akizungumza na Waandishi wa
Habari jana Mjini hapa,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma,Gilles Muroto alisema
wanaendelea kumtafuta dereva huyo kutokana na kuwepo wakati tukio la kupigwa
kwa risasi kwa Lissu linatokea.
“Bado hatujampata lakini tunaendelea kumtafuta
popote alipo tunamwambia tunamtafuta ila bado hatujampata tunaendelea kwa
kuvitumia vyanzo vyetu,”alisema
Alipoulizwa kuhusina na magari
nane aina ya Nissan wanayoyashikiliwa na Jeshi hilo,Kamanda Muroto alisema bado
wanaendelea kuyashikilia mpaka watakawapata wahusika wa tukio hilo.
“Magari tunaendelea kuyashikilia kikubwa
tunataka usaidizi ili tuweze kuweka mambo yetu sawa,”alisema
Kuhusina na ulinzi nyumbani
kwa Lissu,Kamanda Muroto alisema,Usalama upo wa kutosha kutokana na Jeshi hilo kuuimarisha .
“Pia tumeweka Road Bloak, Mji
uko ndani ya bakulia umezibwa na doria za magari na pikipiki sehemu zote za
kutoka na kuingia Dodoma zipo katika doria,”alisema
Alipoulizwa ni kampuni gani
inalinda katika eneo Lissu alipopigiwa risasi,alisema hawezi kujua ila
anachojua ni kwamba kila nyumba ina mlinzi binafsi.
“Kila nyumba ina ulinzi
binafsi lakini ulinzi wa getini upo kama
kawaida sema siwezi kujua ni kampuni gani inafanya ulinzi huo,”
BANDA BLOG ilifika
kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma na kukuta gari la Lissu likiwa nje ya
Jengo hilo huku likiwa limefunikwa upande ambao una matundu ya risasi ambapo pia namba
za gari hiyo zikiwa zimetolewa.
Wakati huo huo Jeshi
linawashikilia watu watano raia wa China kwa kupatikana na nyara za Serikali ambazo ni
Magamba ya 652 ya Kakakuona,Kucha na jino la Simba kinyume cha sheria.
Alisema watuhumiwa hao
walikamatwa Septemba 11 mwaka huu kwa kushirikiana na askari wa kikosi dhidi ya
Ujangili(KDU) Kanda ya Kati Manyoni.
Kamanda Muroto alisema watuhumiwa hao walikamatwa na Magamba 652 ya
mnyama Kakakuona,kucha tano za Kakakuona,kucha nne za Simba, na jino moja la
Simba.
“Katika msako unaoendelea
maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dodoma wamekamatwa watuhumiwa 12 kwa makosa ya
uvunjaji wa nyumba na wizi,maliz ilizokamatwa ni Television Flat Screen 13
Radio Saboofer 2,Speaker 5,Deck ,bhangi kete 12,”alisema
Kamanda Muroto,alitoa wito
kwa wote walioibiwa majumbani mwao kufika katika Kituo cha Polisi cha kati kwa
ajili ya kutambua mali walizoibiwa.
mwisho
Tags
POLISI DOM




