BANDA MEDIA BLOG

IBADA YA EID EL HAJJ YAFANYIKA MJINI DODOMA MASHEKH WAFUNGUKA


Mkuu wa Maimamu wa Msikiti wa Nunge Shekh Ahmed Zuber akifafanua jambo wakati akitoa mawaidha katika uwanja wa jamhuri wakati wa sherehizo

Mawadha yakiendelea

Waumini wa Dini ya Kiiislamu Wakisujudu wakati wa swala hiyo ikiendelea [PICHA NA JOHN BANDA WA BANDA, BLOG


 

Shekh Zuber na Mjukuu wake Baada ya Ibada ya Eid el hajj 2017


JOHN BANDA-DODOMA
MKOANI Dodoma Waislamu wametakiwa kujikita katika malezi ya watoto kwa kuhakikisha wanawapatia elimu ya dini ya kiislamu kwani itawasaidia katika maadili pamoja na kuipenda nchi yao.
Hayo yalilezwa Mjini hapa na Ustadh Abdullaziz Yunus wakati wa Ibada ya swala ya Idd el hajj iliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoani hapa.
Ustadh Yunus ambaye ni Imamu katika Msikiti wa Bilal uliopo Area C Mkoani hapa amesema, wazazi na walezi wanawajibu wa kuhakikisha watoto wanapatiwa Elimu ya dini ya Kiislamu kwani itawasaidia katika maadili pamoja na kuipenda nchi yao.
Amesema kitendo cha wazazi kuwaacha watoto wakiendelea kufanya mambo ambayo ni tofauti na dini kwa kisingizio cha Sayansi na Teknolojia ndio husababisha,watoto hao kuporomoka kimaadili.
Awali Imamu Mkuu wa Msikiti wa Nunge  Shekhe,Ahmed Zuber aliishukuru Serikali kwa kukubali eneo la Kizota liendelee kutumiwa na Waislamu kwa ajili ya maziko.
Wakati huo huo Shekhe wa Jumuiya ya Ahmadiyya Muslim Jamaaat Tanzania Bashart Ur Rehman Butt  amewataka waumini wa dini ya Kiislamu nchini  kuisaidia jamii yenye mahitaji maalumu kuwa ni sehemu ya tendo la ibada la kila siku badala ya kusubiri sherehe za Eid el hajj .
Kiongozi huyo wa dini amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ibada ya swala ya sikukuu ya Eid el hajj
Mbali na hilo amewataka waumini wa dini hiyo kuendelea kudumisha amani upendo na ushirikiano ili maendeleo yanayosisitizwa kwa ajili ya Taifa yaweze kuongezeka na hatimaye tufikia hatua ya kiuchumi wa viwanda na biashara.
mwisho

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG