Milango ya saa 10:00 jioni jumamosi ya Octoba 28, 2017 wapinzani wa jadi nchini katika soka wanakwenda kukutana ndani ya uwanja wa Uhuru katika mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu Tanzania bara . Hawa si wengine bali ni mnyama Simba SC na wana jangwani Yanga SC.
Mchezo huo ni namba tatu Afrika kwa umaarufu katika soka ukitanguliwa na vinara Al Ahly dhidi ya Zamaleki pale jijini Cairo nchini Misri al maarufu kama Caira Derby . Mtanange wa wababe wa ligi kuu nchini Afrika kusini katika viunga vya Soweto Orlando pirates na Kaizer chiefs wanashika namba mbili wakisimama na jina la Soweto derby.
Timu hizi zinakutana huku kila mmoja akiwa na ari, nguvu na hamasa kubwa ya kusaka ushindi ili kujitengenezea njia ya kulinyakua kombe la ligi kuu msimu huu pia kuweka heshima kwa mtani wake. Wote wana wana alama 15 kileleni mwa msimamo wa ligi kuu lakini Simba SC akiongoza jahazi kutokana na wingi wa magoli . Hili peke yake linaleta mvuto wa aina yake kuelekea mchezo huo.
SIMBA SC
Kuelekea mchezo wa jumamosi, wanaonesha hamasa kubwa ya kuibuka wababe katika mtanange huo wa jadi . Upana wa kikosi chao , uwezo wa mchezaji mmoja mmoja , matokeo ya nyuma, uongozi katika ligi vitawafanya kusimama mbele ya Yanga wakiwa na mtaji mzuri wa kisaikolojia kuliko wapinzani wao na endapo wataitumia vyema fursa hiyo wanaweza kuibuka washindi jumamosi.
Msimu huu wa 2017-18 Simba wamefanya usajili mzuri tofauti na misimu kadhaa nyuma toka waliponyakua kombe la ligi kuu kwa mara ya mwisho mwaka 2012. Timu imekuwa na mseto mzuri wa vijana na wakongwe hali inayowafanya kuwa na kikosi kipana kuliko timu yoyote ndani ya ligi kuu kwa sasa . Upana wa kikosi chao ni uwezo unaoshabihana wa mchezaji mmoja mmoja katika kila eneo uwanjani hali inayolifanya benchi la ufundi la timu hiyo kuwa na nafasi kubwa ya kuipanga timu kulingana na mahitaji kwa mchezaji husika pia kutokuwa n hofu ya majeruhi au kuporomoka kwa kiwango cha mchezaji kuhatarisha ufanisi wao.
Mchezo wa mwisho wa Simba SC dhidi ya Mji Njombe walinzi wa kati walisimama Juuko Murshid na Jamali Mlipili aliesajiliwa msimu huu tokea Mbao FC . Akicheza mechi yake ya kwanza ndani ya jezi ya Simba, Mlipili alionesha uwezo mkubwa pembeni ya beki kisiki wa timu ya taifa ya Uganda nafasi ambayo mara nyingi husimama Method Mwanjali na Salimu Mbonde ambaye ni majeruhi. Hii ndio dhana ya upana wa kikosi .
Simba ina wachezaji ambao wana uwezo mkubwa kuamua matokeo ya mechi, kusimama vyema na mfumo na mbinu za mwalimu ili kuipa matokeo chanya timu hiyo endapo bahati ya ushindi itakuwa upande wao.
Ni dhahiri Aishi Manula golikipa namba moja wa timu hiyo na timu ya taifa atakaa langoni siku ya jumamosi Mungu akimjalia afya njema na utimamu wa mwili. Huyu ni golikipa bora wa ligi kuu nchini mara mbili mfululizo na tayari ana uzoefu wa joto la mechi hii akisimama imara langoni mechi ya ufunguzi wa ligi ya Ngao ya jamii dhidi ya Yanga . Manula alipangua penati Kelvin Yondani na kujipanga vyema langoni hali iliyomfanya Juma Mahadhi kujikuta anapaisha mkwaju wa penati na kuwapa ubingwa Simba SC hivyo anaiendea mechi hiyo akiwa vyema kisaikolojia dhidi ya Yanga pia anawajua vyema toka akiwa Azam FC akiwa sehemu ya kikosi kilichoipiga Yanga 4-0 katika mchezo wa Nusu fainali ya michuano ya kombe la Mapinduzi mapema mwaka huu.
Erasto Nyoni ni mchezaji mkongwe ndani ya ligi kuu Tanzania bara na huyu nina imani katika note book ya kocha mkuu wa Yanga SC George Lwandamina lazima yumo kuelekea mchezo huo adhimu kisoka nchini. Erasto ni kiraka eneo lote la ulinzi pia akiwa na uwezo mkubwa kucheza kama kiungo mkabaji. Sifa kubwa mchezaji huyu ni uwezo wa kudumu na kiwango chake ndani ya dakika 90 akicheza kwa kujituma , nguvu , akili ya mpira na kutimiza vyema majukumu yake uwanjani. Akipangwa kama mlinzi wa pembeni basi husimama imara kama mlinzi wa wing pia kiungo wa akiba wa pembeni kulinda n kushambulia. Uwezo wake huo ndio ulimfanya mechi ilyopita dhidi ya Njombe mji kuitengenezea magoli Simba kupitia wing ya kulia akicheza kama mlinzi wa kulia na kiungo wa pembeni. Ana uwezo mkubwa kuibana timu pinzani katika mashambulizi yake ya upande lakini pia akishirikiana vyema na wenzake kupandisha vyema timu . Endapo atapangwa jumamosi beki ya kulia , na benchi la ufundi la Yanga SC kumpanga Mwashiuya kama walivyofanya mechi ya juzi dhidi ya Stand United ni dhahiri kutakuwa na upinzani mkali . Kama Mwashiuya asipokuwa makini kwenye pressing atajikuta mipira mingi anaipoteza kabla ya kupiga krosi au kuukata uwanja . Mechi na Stand walikuwa wakifanya tactical overlapping na Ibrahim Ajibu pale ambapo Mwashiuya akipata mpira alikuwa akikokota kwa kuukata uwanja na Ajibu kutanua pembeni kitu ambacho Erasto ni mkongwe anaweza kuziba njia kwa kusogea juu kwenye edge ya 18 kuziba njia huku akifanya mawasiliano mazuri na walinzi wa kati kwa ajili aidha ya offside trick au covering.
Wengine ni Ally Shomari pia mlinzi wa kulia ambaye anaweza pia kuanza na kusimama vyema katika mechi hiyo , Zimbwe jr kushoto bado ni mwiba mkali katika ulinzi na kupandisha mashambulizi amecheza zaidi ya mechi tano za watani wa jadi hivyo hana pressure . Mkongwe Method Mwanjali kuna uwezekano mkubwa kuanza mechi hiyo akisimama na Juuko. Ana uwezo mzuri sema jazba na hasira za haraka ni kitu cha kuchunga kwake.
Safu ya kiungo ya Simba ndio eneo ambalo Yanga wanatakiwa kulipigia hesabu za mbali kidogo . Hapa ndipo patakapoamua matokeo ya jumamosi aidha sare , kufunga au kufungwa. Msimu uliopita Simba ilikuwa bora eneo la kiungo lakini wakawa butu kwenye safu ya ushambuliaji kwa sababu walikosa mtu wa kuiunganisha timu toka eneo la kiungo kwenda mbele .
Katika soka timu ikiwa bora kwenye ulinzi na kiungo ukaona inapwaya kwenye ushambuliaji kwa maana ya kushindwa kutumia nafasi wanazotengeneza ni dhahiri inamkosa namba 10 ( playmaker ) mwenye uwezo wa kuunganisha kazi za viungo wa kati na pembeni ( technical link up ) kumzunguka mshambuliaji wa kati au kuitanua vyema safu hiyo ili iwe na uwezo wa kutengeneza washambuliaji zaidi ya wawili inapoingia kwenye final third . Ujio wa Emanuel Okwi umetibu vyema tatizo la Simba SC katika hili ndio maana wana uwezo mkubwa wa kufunga . Okwi anasimama kama playmaker na mshambuliaji wa timu hiyo kitu ambacho kinawapa wakati mgumu wapinzani wake .
Si kwamba Omog anatengeneza mfumo wa ushambuliaji wa Simba kumzunguka mchezaji huyo , hapana kiufundi hili ni hatari na kwa uwezo wa kocha huyo sizani kama anaweza kufanya hivyo kwa maana anatambua akibanwa mchezaji huyo patterns zake zinakuwa zimefeli. Mechi na Mji Njombe alimpanga Mzamiru Yassin namba 8 kama kiungo wa juu akicheza sambamba na Jonasi Mkude huku Haruna Niyonzima akicheza wing ya kushoto na Okwi akicheza kama ‘ false 10’ . Kuna mbinu alikuwa anaijaribu Omog kuelekea mchezo wa jumamosi kupitia Njombe mji na kwa kiasi alifanikiwa . Aliwahadaa Mji Njombe kumchezesha Mzamiru kama kiungo mchezeshaji lakini alimpanga kama kiungo mshambuliaji kamili ( kifucho ) . Majukumu ya kuchezesha timu yalikuwa ya Niyonzima akibadili mifumo ya pasi uwanjani , kufunga na kufungua uwanja huku Okwi akitoka kucheza kama namba kumi na kucheza huru kulia na kushoto kwenye final third kama kiungo mshambuliaji namba mbili. 4-3-3 inahitaji viungo washambuliaji zaidi ya wawili. Endapo Yanga wataingia uwanjani kumtazama Okwi tu kwenye safu yao ya ulinzi watakuwa wamekosea na wanaweza kuumia . Umakini unahitajika kwa kuwatizama Simba wanapoanza kutoka nyuma kwenye wings na kati ni akina nani wanaenda timu kabla ya kuingia kwenye eneo lao la ulinzi.
Wapo wengi katika kiungo kwa upande wa Simba ; Ndemla huyu mara nyingi huanzia benchi kutokana na uwezo mkubwa wa kuwasoma wapinzani. Mara kadhaa amekuwa mwiba kwa Yanga kwa kutokea benchi na kubadili matokeo . Matokeo ya 3-3 msimu wa Brandts kwa Yanga huyu ndio alikuja kuikoa Simba wakiwa nyuma kwa goli tatu sambamba na Lucian. Kichuya kulia ni viungo James Kotei na pacha wake Jonasi Mkude ambaye amerudi vyema katika kiwango chake ni watu ambao wanaweza kuichachafya Yanga eneo la kati.
Kwenye ushambuliaji driving force kubwa ya Simba inaanzia kati na kwenye wings . Erasto Nyoni kulia na Zimbwe junior kushoto wana uwezo mkubwa kupanga mashambulizi sambamba na viungo wa pembeni Shiza Kichuya na Haruna Niyonzima ili kuwalisha vyema wachezaji wa kati Emanuel Okwi , Mavugo na Juma Luizio . Yanga kwa sasa si imara sana kwenye wings kama misimu miwili ya nyuma kutokana na kuondokewa na nyota wake kadhaa. Pengo la Saimoni Msuva kulia bado ni kubwa ambaye alikuwa akiwakaba wapinzani kwa kuwashambulia muda wote . Pius Buswita ana kazi ya ziada kuzima kazi ya Zimbwe na Niyonzima kwa jumamosi ili kuwanyima fursa kupitia kwenye wings.
Mabadiliko ya benchi la ufundi kwa kuondoka kocha msaidizi Jakson Mayanja na ujio wa mburundi Masoud Djuma siyapi sana nafasi kuleta badiliko kubwa hususani kimbinu lakini yanaongeza hamasa ya upambanaji bado Simba itatembelea mipango na mbinu za Omog kuliko Masoud ambaye ni kocha msaidizi na bado hajapata muda wa kutosha na timu.
USIKOSE TOLEO LIJALO KUHUSU YANGA SC KATIKA MWENDELEZO WA MAKALA HII…
@ SAMUEL SAMUEL

Milango ya saa 10:00 jioni jumamosi ya Octoba 28, 2017 wapinzani wa jadi nchini katika soka wanakwenda kukutana ndani ya uwanja wa Uhuru katika mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu Tanzania bara . Hawa si wengine bali ni mnyama Simba SC na wana jangwani Yanga SC.
Mchezo huo ni namba tatu Afrika kwa umaarufu katika soka ukitanguliwa na vinara Al Ahly dhidi ya Zamaleki pale jijini Cairo nchini Misri al maarufu kama Caira Derby . Mtanange wa wababe wa ligi kuu nchini Afrika kusini katika viunga vya Soweto Orlando pirates na Kaizer chiefs wanashika namba mbili wakisimama na jina la Soweto derby.
Timu hizi zinakutana huku kila mmoja akiwa na ari, nguvu na hamasa kubwa ya kusaka ushindi ili kujitengenezea njia ya kulinyakua kombe la ligi kuu msimu huu pia kuweka heshima kwa mtani wake. Wote wana wana alama 15 kileleni mwa msimamo wa ligi kuu lakini Simba SC akiongoza jahazi kutokana na wingi wa magoli . Hili peke yake linaleta mvuto wa aina yake kuelekea mchezo huo.
SIMBA SC
Kuelekea mchezo wa jumamosi, wanaonesha hamasa kubwa ya kuibuka wababe katika mtanange huo wa jadi . Upana wa kikosi chao , uwezo wa mchezaji mmoja mmoja , matokeo ya nyuma, uongozi katika ligi vitawafanya kusimama mbele ya Yanga wakiwa na mtaji mzuri wa kisaikolojia kuliko wapinzani wao na endapo wataitumia vyema fursa hiyo wanaweza kuibuka washindi jumamosi.
Msimu huu wa 2017-18 Simba wamefanya usajili mzuri tofauti na misimu kadhaa nyuma toka waliponyakua kombe la ligi kuu kwa mara ya mwisho mwaka 2012. Timu imekuwa na mseto mzuri wa vijana na wakongwe hali inayowafanya kuwa na kikosi kipana kuliko timu yoyote ndani ya ligi kuu kwa sasa . Upana wa kikosi chao ni uwezo unaoshabihana wa mchezaji mmoja mmoja katika kila eneo uwanjani hali inayolifanya benchi la ufundi la timu hiyo kuwa na nafasi kubwa ya kuipanga timu kulingana na mahitaji kwa mchezaji husika pia kutokuwa n hofu ya majeruhi au kuporomoka kwa kiwango cha mchezaji kuhatarisha ufanisi wao.
Mchezo wa mwisho wa Simba SC dhidi ya Mji Njombe walinzi wa kati walisimama Juuko Murshid na Jamali Mlipili aliesajiliwa msimu huu tokea Mbao FC . Akicheza mechi yake ya kwanza ndani ya jezi ya Simba, Mlipili alionesha uwezo mkubwa pembeni ya beki kisiki wa timu ya taifa ya Uganda nafasi ambayo mara nyingi husimama Method Mwanjali na Salimu Mbonde ambaye ni majeruhi. Hii ndio dhana ya upana wa kikosi .
Simba ina wachezaji ambao wana uwezo mkubwa kuamua matokeo ya mechi, kusimama vyema na mfumo na mbinu za mwalimu ili kuipa matokeo chanya timu hiyo endapo bahati ya ushindi itakuwa upande wao.
Ni dhahiri Aishi Manula golikipa namba moja wa timu hiyo na timu ya taifa atakaa langoni siku ya jumamosi Mungu akimjalia afya njema na utimamu wa mwili. Huyu ni golikipa bora wa ligi kuu nchini mara mbili mfululizo na tayari ana uzoefu wa joto la mechi hii akisimama imara langoni mechi ya ufunguzi wa ligi ya Ngao ya jamii dhidi ya Yanga . Manula alipangua penati Kelvin Yondani na kujipanga vyema langoni hali iliyomfanya Juma Mahadhi kujikuta anapaisha mkwaju wa penati na kuwapa ubingwa Simba SC hivyo anaiendea mechi hiyo akiwa vyema kisaikolojia dhidi ya Yanga pia anawajua vyema toka akiwa Azam FC akiwa sehemu ya kikosi kilichoipiga Yanga 4-0 katika mchezo wa Nusu fainali ya michuano ya kombe la Mapinduzi mapema mwaka huu.
Erasto Nyoni ni mchezaji mkongwe ndani ya ligi kuu Tanzania bara na huyu nina imani katika note book ya kocha mkuu wa Yanga SC George Lwandamina lazima yumo kuelekea mchezo huo adhimu kisoka nchini. Erasto ni kiraka eneo lote la ulinzi pia akiwa na uwezo mkubwa kucheza kama kiungo mkabaji. Sifa kubwa mchezaji huyu ni uwezo wa kudumu na kiwango chake ndani ya dakika 90 akicheza kwa kujituma , nguvu , akili ya mpira na kutimiza vyema majukumu yake uwanjani. Akipangwa kama mlinzi wa pembeni basi husimama imara kama mlinzi wa wing pia kiungo wa akiba wa pembeni kulinda n kushambulia. Uwezo wake huo ndio ulimfanya mechi ilyopita dhidi ya Njombe mji kuitengenezea magoli Simba kupitia wing ya kulia akicheza kama mlinzi wa kulia na kiungo wa pembeni. Ana uwezo mkubwa kuibana timu pinzani katika mashambulizi yake ya upande lakini pia akishirikiana vyema na wenzake kupandisha vyema timu . Endapo atapangwa jumamosi beki ya kulia , na benchi la ufundi la Yanga SC kumpanga Mwashiuya kama walivyofanya mechi ya juzi dhidi ya Stand United ni dhahiri kutakuwa na upinzani mkali . Kama Mwashiuya asipokuwa makini kwenye pressing atajikuta mipira mingi anaipoteza kabla ya kupiga krosi au kuukata uwanja . Mechi na Stand walikuwa wakifanya tactical overlapping na Ibrahim Ajibu pale ambapo Mwashiuya akipata mpira alikuwa akikokota kwa kuukata uwanja na Ajibu kutanua pembeni kitu ambacho Erasto ni mkongwe anaweza kuziba njia kwa kusogea juu kwenye edge ya 18 kuziba njia huku akifanya mawasiliano mazuri na walinzi wa kati kwa ajili aidha ya offside trick au covering.
Wengine ni Ally Shomari pia mlinzi wa kulia ambaye anaweza pia kuanza na kusimama vyema katika mechi hiyo , Zimbwe jr kushoto bado ni mwiba mkali katika ulinzi na kupandisha mashambulizi amecheza zaidi ya mechi tano za watani wa jadi hivyo hana pressure . Mkongwe Method Mwanjali kuna uwezekano mkubwa kuanza mechi hiyo akisimama na Juuko. Ana uwezo mzuri sema jazba na hasira za haraka ni kitu cha kuchunga kwake.
Safu ya kiungo ya Simba ndio eneo ambalo Yanga wanatakiwa kulipigia hesabu za mbali kidogo . Hapa ndipo patakapoamua matokeo ya jumamosi aidha sare , kufunga au kufungwa. Msimu uliopita Simba ilikuwa bora eneo la kiungo lakini wakawa butu kwenye safu ya ushambuliaji kwa sababu walikosa mtu wa kuiunganisha timu toka eneo la kiungo kwenda mbele .
Katika soka timu ikiwa bora kwenye ulinzi na kiungo ukaona inapwaya kwenye ushambuliaji kwa maana ya kushindwa kutumia nafasi wanazotengeneza ni dhahiri inamkosa namba 10 ( playmaker ) mwenye uwezo wa kuunganisha kazi za viungo wa kati na pembeni ( technical link up ) kumzunguka mshambuliaji wa kati au kuitanua vyema safu hiyo ili iwe na uwezo wa kutengeneza washambuliaji zaidi ya wawili inapoingia kwenye final third . Ujio wa Emanuel Okwi umetibu vyema tatizo la Simba SC katika hili ndio maana wana uwezo mkubwa wa kufunga . Okwi anasimama kama playmaker na mshambuliaji wa timu hiyo kitu ambacho kinawapa wakati mgumu wapinzani wake .
Si kwamba Omog anatengeneza mfumo wa ushambuliaji wa Simba kumzunguka mchezaji huyo , hapana kiufundi hili ni hatari na kwa uwezo wa kocha huyo sizani kama anaweza kufanya hivyo kwa maana anatambua akibanwa mchezaji huyo patterns zake zinakuwa zimefeli. Mechi na Mji Njombe alimpanga Mzamiru Yassin namba 8 kama kiungo wa juu akicheza sambamba na Jonasi Mkude huku Haruna Niyonzima akicheza wing ya kushoto na Okwi akicheza kama ‘ false 10’ . Kuna mbinu alikuwa anaijaribu Omog kuelekea mchezo wa jumamosi kupitia Njombe mji na kwa kiasi alifanikiwa . Aliwahadaa Mji Njombe kumchezesha Mzamiru kama kiungo mchezeshaji lakini alimpanga kama kiungo mshambuliaji kamili ( kifucho ) . Majukumu ya kuchezesha timu yalikuwa ya Niyonzima akibadili mifumo ya pasi uwanjani , kufunga na kufungua uwanja huku Okwi akitoka kucheza kama namba kumi na kucheza huru kulia na kushoto kwenye final third kama kiungo mshambuliaji namba mbili. 4-3-3 inahitaji viungo washambuliaji zaidi ya wawili. Endapo Yanga wataingia uwanjani kumtazama Okwi tu kwenye safu yao ya ulinzi watakuwa wamekosea na wanaweza kuumia . Umakini unahitajika kwa kuwatizama Simba wanapoanza kutoka nyuma kwenye wings na kati ni akina nani wanaenda timu kabla ya kuingia kwenye eneo lao la ulinzi.
Wapo wengi katika kiungo kwa upande wa Simba ; Ndemla huyu mara nyingi huanzia benchi kutokana na uwezo mkubwa wa kuwasoma wapinzani. Mara kadhaa amekuwa mwiba kwa Yanga kwa kutokea benchi na kubadili matokeo . Matokeo ya 3-3 msimu wa Brandts kwa Yanga huyu ndio alikuja kuikoa Simba wakiwa nyuma kwa goli tatu sambamba na Lucian. Kichuya kulia ni viungo James Kotei na pacha wake Jonasi Mkude ambaye amerudi vyema katika kiwango chake ni watu ambao wanaweza kuichachafya Yanga eneo la kati.
Kwenye ushambuliaji driving force kubwa ya Simba inaanzia kati na kwenye wings . Erasto Nyoni kulia na Zimbwe junior kushoto wana uwezo mkubwa kupanga mashambulizi sambamba na viungo wa pembeni Shiza Kichuya na Haruna Niyonzima ili kuwalisha vyema wachezaji wa kati Emanuel Okwi , Mavugo na Juma Luizio . Yanga kwa sasa si imara sana kwenye wings kama misimu miwili ya nyuma kutokana na kuondokewa na nyota wake kadhaa. Pengo la Saimoni Msuva kulia bado ni kubwa ambaye alikuwa akiwakaba wapinzani kwa kuwashambulia muda wote . Pius Buswita ana kazi ya ziada kuzima kazi ya Zimbwe na Niyonzima kwa jumamosi ili kuwanyima fursa kupitia kwenye wings.
Mabadiliko ya benchi la ufundi kwa kuondoka kocha msaidizi Jakson Mayanja na ujio wa mburundi Masoud Djuma siyapi sana nafasi kuleta badiliko kubwa hususani kimbinu lakini yanaongeza hamasa ya upambanaji bado Simba itatembelea mipango na mbinu za Omog kuliko Masoud ambaye ni kocha msaidizi na bado hajapata muda wa kutosha na timu.
USIKOSE TOLEO LIJALO KUHUSU YANGA SC KATIKA MWENDELEZO WA MAKALA HII…
@ SAMUEL SAMUEL