Mkuu wa zamani wa vikosi vya ulinzi Zimbabwe aapishwa; Mugabe nae apatiwa haki za kidiplomasia
Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ambaye ameahidi kutekeleza marekebisho ya kiuchumi na kisiasa nchini, jana alimpatia pia Rais aliyemtangulia wa nchi hiyo mwenye umri wa miaka 93 Robert Mugabe haki kamili ya kidiplomasia. Ni vyema kuashiria hapa kuwa Mugabe amekuwa akiishi katika nyumba yake binafsi katika eneo la Borrowdale huku malipo yake ya kiinua mgongo yakimhainishia malipo ya donge nono la fedha yaliyo na thamani sawa na nyumba binafsi.
Rais Mnangagwa wa Zimbabwe amebainisha kuwa marais wa zamani waliohudumu kwa uchache kipindi kimoja kizima; mchanganuo ambao unamjumuisha Mugabe pekee wanapasa pia kupatiwa walinzi sita na ofisi yenye samani kamili. Licha ya kutekeleza hayo yote, Rais mpya wa Zimbabwe anakabiliwa na mashinikizo kutoka kwa wawekezaji wa nje, vyama vya upinzani na wananchi wa kawaida wa Zimbabwe ili kutekeleza mageuzi ya kiuchumi aliyoahidi nchini humo. Mnangagwa aliapishwa kuwa rais mpya wa Zimbabwe tarehe 24 Novemba, siku tatu baada ya rais wa zamani wa nchi hiyo, Robert Mugabe kutangaza kujiuzulu kufuatia mashinikizo ya kila upande.
Tags
Zimbabwe ya Mugabe