2017 ndio huoo umebakiza siku chache kuisha huku Kylian
Mbappe akiwa jina lililoushtua ulimwengu, lakini 2018 kuna vijana wadogo
ambao wanaweza kufanya kile Mbappe alichofanya 2017.

1.Phil Foden,ana miaka 17 raia wa Uingereza na tayari msimu huu katika
mechi kadhaa alionekana akiwa benchi la Man City, Pep ameanza kuona
ukubwa wa Foden na katika fainali za vijana under 17 alifunga mara
mbili.

2.Justin Kluivert, pengine kwa sasa anazungumziwa sana huku
akihusishwa na kwenda Manchester United, mtoto wa nyota wa zamani wa
Barca Patrick Kluivert anatajwa kama nyota tishio zaidi katika siku za
usoni
.

3.Ferran
Torres, ni habari kubwa nchini Hispania na huyu ndio mchezaji wa kwanza
kuzaliwa kuanzia mwaka 2000 na kucheza La Liga, mkataba wake na
Valencia unakaribia kuisha huku Barcelona na Real Madrid wakifuatilia
kwa karibu hatma yake.

4.Jadon
Sancho, alizaliwa mwaka 2000 akakulia kituo cha kulea wachezaji cha Man
City na baadae aliamua kutafuta timu, alizitosa United na Chelsea
baadae akatua Dortmund ambako anapewa nafasi kumrithi Dembele na tayari
watabiri wa mambo wanasema Sancho ni almasi kubwa ijayo katika soka.

5.Ethan
Ampadu, inajulikana kwamba Antonio Conte haamini watoto huwa anapenda
wazee wa kazi, lakini sio kwa Ampadu ambaye ana miaka 17 tu huku tayari
Conte ameshampa nafasi na anaonekana kumkubali, ni kijana ambaye anaweza
kuwa lulu mpya Chelsea.