
Majengo hayo yaliyojengwa na TBA kwa miezi minane yakielezwa kugharimu Sh10 bilioni yalizinduliwa Aprili 15,2017.
Ujenzi ulifanyika ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kumaliza tatizo la malazi kwa wanafunzi wa UDSM.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga, jana alisema hata yeye ameziona picha hizo kwenye mitandao ya kijamii.
“Nimeziona na muda huu najiandaa kwenda huko kuangalia kama taarifa hizo ni za kweli,” al;isema Mwakalinga
Picha hizo zilianza kusambaa jana jioni. Mwakalinga alisema huenda picha hizo ni za majengo mengine lakini zimehusishwa na hosteli hizo.
“Nitatoa taarifa baada ya kukagua majengo hayo kwa sasa siwezi kuzungumza hadi nitakapoona,” alisema.
