BANDA MEDIA BLOG

KESI YA SUGU KIZUNGUMKUTI, AKOSA ZAMANA ARUDISHWA RUMANDE



MBEYA: Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama SUGU amekosa dhamana baada ya mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi kusema kuwa inataka kumaliza kesi yake mapema na kwa muda mfupi na pia sugu huwa anatabia ya kutohudhuria mahakamani kwa wakati.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Mbeya Michael Mtaite amesema sababu ya kumnyima dhamana mshtakiwa Mh. Mbilinyi na mwenzake ambaye ni katibu wa CHADEMA kanda ya nyanda za juu kusini Emmanuel Masonga ni hofu ya mshtakiwa kutohudhuira mahakamani mara kwa mara na pia anataka kesi hiyo isikilizwe siku chache na kwa mfufulizo iwe imekwisha.



"Mahakama inataka kusikiliza kesi hii kwa muda mfupi sana, ndani ya wiki moja kuanzia jumatatu iwe imeshakwisha, hivyo tunawataka washtakiwa kurudi rumande" alisema Mtaite


Sugu na mwezake wanashtakiwa kwa kutoa lugha za uchocheza na za fedhiha kwa Rais Magufuli mnamo tarehe 30,Desemba mwaka jana katika viwanja vya mwenge jijini mbeya.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG