Watu wasipoungua 43 wameuawa katika kipindi ccha siku moja iliyopita nchini Marekani katika matukio ya ufyatulianaji risasi nchini humo.
Kwa mujibu wa takwimu za Mashambulio ya Bunduki nchini Marekani, watu hao wameuawa katika majimbo ya Texas,Missouri, Minnesota, Florida, Illinois na Alabama
Takwimu zinaonyesha kuwa katika vitendo 110 vya ufatulianaji risasi kati ya Ijumaa na Jumamosi, watu 43 waliuawa na wengine 64 kujeruhiwa.
Kwa mujibu wa Kituo cha Takwimu za Mashambulio ya Bunduki Marekani mwaka 2017, kulikuwa na matukio 61,000 ya ufyatulianaji risasi kiholela nchini humo.
Tags
Mauaji