Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli atazindua Chuo cha
Mafunzo Maalum ya Kijeshi kilichopo Mapinga Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa
Pwani kesho tarehe 06 Februari 2018 kuanzia saa 01:45 asubuhi.
Ukiwa mdau muhimu wa habari, chombo chako kinaalikwa kuhudhuria katika tukio hilo muhimu.
Usafiri wa kwenda chuoni Mapinga
utapatikana Mwenge kituo cha Mafuta cha PUMA kuanzia saa 12:30 asubuhi
na safari itaanza saa 01:00 asubuhi.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
05 Februari, 2018.
Tags
RAIS MAGUFULI