![]() |
| Waziri TAMISEMI Suleman Jafo akifafanua jambo katika uzinduzi huo |
![]() |
| Waziri Jaffo, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Wizara ya Afya Margeret Mussai wakiwa pamoja na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kwenye uzinduzi huo, [PICHA NA JOHN BANDA WA BANDA BLOG] |
![]() |
| Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM [UVCCM]Mkoa wa Dodoma Billy Chidambwa akisalimia katika uzinduzi huo |
![]() |
| Mkurugenzi Mtendaji wa Creative Plan akizungumza kwenye uzinduzi huo |
![]() |
| Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Wizara ya Afya Margeret Mussai |
NA JOHN BANDA, DODOMA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Sulemani Jaffo amewataka walimu kote nchini kutunga nyimbo za Mchaka Mchaka watakazokuwa wakitumia wanafunzi zinataja Rushwa hali itakayowafanya watanzania kuchukia Rushwa kuanzia wakiwa wadogo
Jaffo alitoa agizo hilo kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Kupambana na Rushwa na Mimba za Utotoni kupitia Club za wanafunzi wa Msingi na Sekondari mashuleni kampeni inayoendeshwa na Wizara ya Afya na Shiriki la Creative Plan [CP]
"watoto hawa wakiwa wanaimba nyimbo za mchaka mchaka na huku wakiitaja rushwa na madhara yake kwa jamii ya Watanzania, itaeleweka zaidi na itasikika vizuri hata kwa wali ambao hawataki kiisikia masikiaoni mwao na hivyo itakuwa rahisi kuikabili watakapokuwa wakubwa walimu wasaidini", alisema
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali la CREATIVE PLAN Juma Mtewa alisema ni rahisi kumfundisha mtoto kuliko mtu mzima kwa kuwa Mtu mzima hawezi kuelewa kwa haraka kama ilivyo kwa mtoto
"Kazi hii ni muhimu sana kwa taifa tunamshukuru Waziri Jaffo kwa kuwatangazia Wakuu wa Mkoa ili watupe ushirikiano lakini imekuwa na changamoto kubwa kwa kuwa wengine wanajua kunakuwa na posho na tunapowambia ni kujitolea wanakimbia hapa tulipo tupo wenyewe viongozi mbalimbali walituacha lakini pia wapo wengine wanaojua kuwa tumekuja kuwachimba hivyo changamoto ni kubwa", alisema
Nae Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto wa Wizara ya Afya Margaret Mussai aliwataka wazazi, walezi pamoja na jamii kwa ujumla kuhakikisha wanawaweka watoto kwenye uangalizi ili kuwaepusha na mimba za utotoni kutoka kwa watu wazima wanaoisha bila kufuata maadili ambao wamekuwa wakiwarubuni watoto kufanya nao ngono kwa vishawishi mbalimbali vikiwemo usafiri, chips na tupesa kidogo kwa ajili ya matumizi shuleni
Tags
RUSHWA











