BANDA MEDIA BLOG

KIGWANGALLA KUTOJIBU MAOMBI YOYOTE YALIYOWASILISHWA OFISINI KWAKE NA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA



WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla, amesema  hatajibu maombi yoyote yaliyowasilishwa ofisini kwake kutoka kwa  wakuu wa mikoa, halmashauri pamoja na  wakuu wa wilaya  ya kufuta  maeneo ya hifadhi, ili maeneo hayo  yatumike kwa ajili ya  matumizi mengine.

Amesema maeneo hayo yalitengwa kisheria na yana umuhimu mkubwa kiuchumi na kijamii, hivyo lazima yaendelee kuhifadhiwa kwa ajili ya faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Amesema katika kipindi cha uwaziri wake hatajibu ombi lolote lile linalohusu kubadili matumizi ya maeneo hayo kwa vile kuwa na misitu sehemu za mijini ni sehemu ya maendeleo.

Aliyasema hayo jana mjini Iringa alipokuwa akizungumza  kwa mara ya kwanza na kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu iliyokutana kwa ajili ya kufanya kikao chake cha tatu tangu ilipoundwa mwaka jana, ikiwa pamoja na kutembelea msitu wa Hifadhi wa Kihesa Kilolo uliombwa na uongozi wa mkoa kufutwa, ili upate kutumika kwa kuweka miundombinu mipya ya mji wa kitalii.

Katika kikao hicho ambacho Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alishiriki, Waziri Kigwangallah  alimuomba mkuu  huyo awafikishie ujumbe   wakuu wa mikoa wengine  ambao walituma na wanaotarajia kutuma maombi ya namna hiyo kuwa yeye  hatakaa hayajibu hadi pale  tu yule  aliyemteua ampe maelekezo na si  vinginevyo.

Alisema  halmashauri nyingi nchini kila zikiona maeneo ya hifadhi zimekuwa zikifikiria kubadili matumizi ya  maeneo hayo, ili yatumike kwa shughuli zingine za maendeleo kama vile  kupima viwanja  ili  kuwauzia wananchi kwa lengo la kukusanya mapato.

"Ofisini kwangu kuna  maombi mengi mno ambayo hata sielewi nianze na lipi na niache lipi, nasema sitajibu ombi lolote lile," alisisitiza Kigwangalla.

Waziri Kigwangallah baada ya kuzungumza na kamati hiyo, alitembelea eneo la hifadhi ya msitu huo  huku  akiwa ameongoza na kamati hiyo  pamoja na Uongozi wa Mkoa wa huo.

Katika ziara hiyo, Kigwagwalla aliwashukia viongozi wa Halmashauri  kwa kuanzisha dampo katika  eneo hilo,  huku kamati ikijionea magari matatu ya taka  yakiendelea kumwaga uchafu kwenye eneo hilo jambo ambalo ni  kinyume cha sheria za uhifadhi.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG