Mshambuliaji wa Manchester City, Raheem Sterling akikosa bao la wazi
kipindi cha pili katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya wenyeji,
Burnley leo Uwanja wa Turf Moor timu hizo zikitoka sare ya 1-1. Man City
ilitangulia kwa bao la Danilo dakika ya 22 kabla ya Johann Berg
Gudmundsson kuisawazishia Burnley dakika ya 82.