![]() |
| Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Bahi Rachel Chuwa akipanda mti kati zoezi hilo |
![]() |
| Afsa Tarafa wa Tarafa hiyo na hakuwa nyuma |
NA JOHN BANDA, DODOMA
Katika
kuunga mkono Agizo la Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan la upandaji wa
miti ili kuukijanisha Mkoa wa Makao makuu ya Nchi – Dodoma mkoa huo umeandaa mkakati wa kuzitaka
Halmashari zote za Wilaya kupanda miti mil 1.5 ambapo ili kufanikisha zoezi
hilo mkuu wa wilaya ya Bahi Elizabert
Kitundu ameagiza kila kata kupanda miti Elfu 70.
Akizungumza
katika uzinduzi wa kampeni ya zoezi hilo la upandaji wa miti uliyofanyika
katika kijiji cha Bahi Sokoni ambapo viongozi mbalimbali walipanda miti Mkuu
huyo wa Wilaya alisema kuwa ili kufanikisha zoezi hilo inabidi kila kijiji
kipande miti 25,400 kwa vijiji vyote 59
“mkoa
umepanga siku hii ya feb 8 iwe siku maalum ya upandaji miti ktk kila wilaya ili
kuunga mkono agizo la serikali na kwetu hapa tunatakiwa kupanda miti million
1.5 na naagiza kila kiongozi wa kata na vijiji atenge eneo la kupanda miti hiyo
Itakuwa kila
nitakapotembelea naomba nionyeshwe miti iliyopandwa na kiongozi yoyote ambaye
hata fanya hivyo hatutamvumilia”, alisema
Awali
akizungumza katika uzinduzi wa mpango huo wa upandaji wa miti hiyo Afsa Aridh
wa Wilaya ya Bahi Chedieli Mrutu amesema ili kuweza kutekeza kwa ufanisi agazo
hilo tayari wameshaanza kushirikisha taasisi na mashirika mengine zikiwemo za
Dini na Tasaf ambao tayari wameshaanza kupanda miti katika baadhi ya vijiji.
Tags
MITI BAHI






