BANDA MEDIA BLOG

SERIKALI YASEMA KAMA SIYO KUINGANISHA MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII PSPF UNGEJIFIA DES MWAKA HUU, KUTOKANA NA KUTOA MAFAO YA 77 BIL. KWA MWEZI HUKU IKIKUSANYA 44 BIL. TU KWA KIPINDI KAMA HICHO

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu Jenista Mhagama akifafanua jambo wakati alipokuwa akiongea na Wajumbe wa Baraza kuu la Chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa [TALGWU], waliokutana kwa ajili ya mkutano wao wa mwaka mjini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu Jenista Mhagamaakiwa pamoja na viongozi wa Chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa TALGWU, wakiamba wimbo wa mshikamano kabla ya waziri huyo kutoa hotuba kwa wajumbe wa Baraza Kuu wa chama hichi waliokutana mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa chama hicho Suleiman  Kikingo akizungumza jambo kabla ya kumkaribisha Waziri Mhagama kuzungumza na wajumbe wa baraza kuu la TALGWU walikutana kufanya mkutano wa mwaka mjini Dodoma  [PICHA ZOTE NA JOHN BANDA WA BANDA BLOG]
 
 











WAZIRI wa Nchi Ofisi ya waziri mkuu, Kazi, Ajira, vijana na walemavu Jenista Mhagama amesema Serikali isingefanya maamuzi ya kuunganisha mifuko ya Hifadhi ya Jamii sekta ya hiyo ilikuwa ina kwenda kufa.
Akizungumza na wajumbe wa baraza kuu la Chama cha wafanyakazi wa Serikali za mitaa [Talgwu] waliokutana mjini Dodoma kwa ajili ya mkutano wao wa mwaka Waziri Mhagama amesema mfuko wa kwanza kufa ungekuwa PSPF  ukifuatiwa na LAPF ambao ungekufa mwezi Desemba mwaka huu kutokana na kukusanya 44 bil kwa mwezi wakati malipo ya pensheni kwa mwezi ni 77 bil.

Aidha Waziri huyo amesema moja ya faida atakazozipata mfanyakazi ni pamoja na kulipwa fedha katika kipindi cha miezi 6 na pia kuweza kuzitoa fedha hizi na kuzihamisha ambapo itakuwa ni faida mara mbili.

Awali akiongea wakati akimkaribisha mgeni rasmi katika mkutano wa Baraza hilo Mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi wa Serikali za mitaaa [Talgwu] Suleiman Kikingo ameainisha shuhuli za mkutano huo wa mwaka uliowakutanisha wajumbe toka mkoa yote ya Tanzania Bara

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG