![]() |
| Jengo la Utawara Chuo kikuu cha Dodoma |
NA JOHN BANDA, UDOM
Wanafunzi wanaosomea Ualimu katika chuo kikuu cha Dodoma [UDOM] wametakiwa kuacha kuchati kwenye Mitandao ya Kijamii kwa ajili ya mambo yasiyofaa yakiwemo mapenzi badala yake waende kwenye shule zilizopo pembezoni mwa chuo hicho kujitolea kufundisha wanafunzi.
Wanafunzi wanaosomea Ualimu katika chuo kikuu cha Dodoma [UDOM] wametakiwa kuacha kuchati kwenye Mitandao ya Kijamii kwa ajili ya mambo yasiyofaa yakiwemo mapenzi badala yake waende kwenye shule zilizopo pembezoni mwa chuo hicho kujitolea kufundisha wanafunzi.
Hayo yamesemwa na Mwanzilishi
na Mratibu wa wanafunzi wa kujitolea wa kitivo cha Elimu Chuo Kikuu cha Dar es-
salaam Emijidius Cornel wakati akizungumza na waandishi wa habari alipokuwa
Chuo kikuu cha Dodoma kwa lengo la kuanzisha tawi la mpango huo wa kujitolea katika ufundishaji wakati wanapokuwa hawana vipindi.
Cornel alisema kuwa katika Collage hiyo iliyopo UDZM walianza wakiwa wanafunzi 10 na kufikia 400 kwa sasa ambapo wanajitolea kufundisha masomo ya Sayansi na Hesabu katika shule za Ilala jijini Dar es salaam na hivyo ujio wake Dodoma ni ili kuanzisha ushirikiano na UDOM
"unajua unaweza kufikili kuna ugumu kujitolea kwenda kufundisha kwa sababu sisi ni wanafunzi wa elimu ya juu hapana hakuna ugumu wowote kwa sababu tunatumia nafasi zile ambazo hatuna vipindi au kama tuna kupindi kimoja tukimaliza tunaenda kujitolea kufundisha wadogo zetu
"unajua unaweza kufikili kuna ugumu kujitolea kwenda kufundisha kwa sababu sisi ni wanafunzi wa elimu ya juu hapana hakuna ugumu wowote kwa sababu tunatumia nafasi zile ambazo hatuna vipindi au kama tuna kupindi kimoja tukimaliza tunaenda kujitolea kufundisha wadogo zetu
"kuna faida kwa mwanafunzi wanaosoma Elimu ya juu kujitolea kufundisha watoto wa shule zinazozunguka Chuo kwa kuwa wanapata uzoefu wa kile wanachosomea kuliko kusubili masomo ya vitendo pekee pia tunashauri wanafunzi wanaosomea fani zingine kwenda kujitolea kutokana na fani zao ili wapate uzoefu", alisema
Kwa upande wake Rais wa
wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma Fransisco Zalalila alimesema anasikitishwa na
Mkoa huo kuwa duni kielimu nchini wakati kuna vyuo vingi vya Elimu ya juu hali inayosababishwa na kutokana kwa taasisi hizo za kielimu kwenda kusaidia jamii inayowazunguka
"ona mkoa wa Dodoma ambao una vyuo vingi vya elimu ya juu lakini bado ufaulu wa wanafunzi wa msingi na sekondari upo chini kitaifa hali hii haikubaliki imefika wakati wanafunzi wa vyuo kujitoa tukawafundishe kwa kujitolea ili kuinua ufaulu ", aliema
Aidha alisema mara baada ya kumaliza mazungumzo na uongozi wa chuo ambao watakutana kuwapa pendekezo lao itawabidi kuuona uongozi wa mkoa kupitia mkuu wa mkoa ili waweze kupata sapoti itakayowarahisishia kufanya kazi hiyo.
Aidha alisema mara baada ya kumaliza mazungumzo na uongozi wa chuo ambao watakutana kuwapa pendekezo lao itawabidi kuuona uongozi wa mkoa kupitia mkuu wa mkoa ili waweze kupata sapoti itakayowarahisishia kufanya kazi hiyo.
Tags
UDOM



