BANDA MEDIA BLOG

NAPE "WANAOTAKA KUBADILI UKOMO WA MADARAKA NI USHETANI"

 


Dar es Salaam: Mbunge wa Mtama mkoa wa Lindi(CCM), Nape Nnauye amesema ulevi wa baadhi Wa viongozi wa Afrika kutamani na kubadili ukomo wa wao kuwa madarakani ni ushetani.

Amesema hayo leo Machi 5, 2018, Kupitia ukurasa wake wa twitter Nape ameandika kuwa ni lazima ushetani huo upingwe kwa nguvu zote hasa na vijana kabla haujaota mizizi na kusambaa. “Huu ulevi wa baadhi ya viongozi wa Afrika kutamani na kubadili ukomo wa wao kuwa madarakani ni ushetani na lazima upingwe kwa nguvu zote hasa na vijana kabla utaratibu huu haujaota mizizi na kusambaa! Hii ni zaidi ya kansa!” aliandika Nape

Nape amewahi kuwa waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kabla ya kuvuliwa wadhifa huo na Rais John Magufuli na nafasi yake kuchukuliwa na Dk Harrison Mwakyembe tulipompigia Muakilishi.com amekiri kuwa twitter ni yake ingawa hakuwa tayari kufafanua zaidi.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG