Wiki iliyopita serikali ya nchi hiyo iliamrisha kufungwa kwa makanisa zaidi ya 700 kwa madai ya kutotimiza kanuni za ujenzi wa makanisa yao.
Miongoni mwa waliokamatwa ni kasisi Askofu Innocent Rugagi, kiongozi wa kanisa la "Abacunguwe" ambaye ni mojawapo ya wachungaji mashuhuri nchini Rwanda.
Polisi inawashutumu kwa kufanya mikutano ya siri kukaidi uamuzi wa serikali.
Ni hivi karibuni serikali iliyapiga marufuku makanisa zaidi ya 700 kwa kukosa miundo mbinu msingi na yalituhumiwa kusababisha kelele nyingi .
Askofu Rugagi alisikika akishutumu kile alichokitaja kuwa uamuzi wa ghafla kuyafunga makanisa bila ya ilani ya kutosha.
Wachungaji hao wamekamatwa baada ya rais Paul Kagame wiki iliyopita kushutumu wazi kile analichokitaja kuwani idadi kubwa ya makanisa haramu nchini.
Kiongozi huyo aliuliza iwapo makanisa hayo, kwa maneno yake, yana manufaa yoyote kuwepo.
Tags
MAKANISA