BANDA MEDIA BLOG

VICENT MBILINYI AJINOWA KUMKABILI HUSSEIN SHEMDOE MEI MOSI TANDIKA



Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ kulia akimnoa bondia Vicent Mbilinyi kwa kumuelekeza kupiga ngumi ya mkunjo wa chini ‘Upcat’ Mbilinyi anajiandaa na mpambano kati yake na Hussein Shemdoe utakaofanyika katika ukumbi wa Musoma Bar siku ya Mei Mosi Picha na SUPER D BOXING NEWS
…………………………………………………………………….
BONDIA Vicent Mbilinyi amendelea na mazoezi ya kumkabili Hussein Shemdoe wakati wa mpambano wao utakaofanyika mei mosi siku ya sikukuu ya wafanyaklazi Duniani mpambano huo utafanyika katika ukumbi wa Musoma Bar uliopo Tandika Mwembe Yanga ambao utakuwa ni  wa raundi 8
Mbilinyi anaenolewa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ amekuwa nje ya ulingo kwa muda wa mwaka mzima sasa tangu mwishoni mwa mwaka 2016 na sasa anakuja kivingine katika masumbwi.
Mbali na mpambano huo siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya mabondia mbali mbali ambapo bondia Shafii Ramadhani atapambana na Antony Mathias wakati Nassibu Ramadhani atavaana na Hamisi Mohamed na Shomari Galibu atapambana na Hashimu Sheni wakati Said Mluguru atavaana na Said Bakari ‘Kidedea’ 
Mapambano haya yote yatafanyika siku hiyo katika ulingo mpya  wa mdau wa masumbwi nchini Zahoro Maganga ‘Super Diego’ aliejenga ulingo huo kwa ajili ya kuwakomboa mabondia kutokana na adha ambayo imekuwa ikijitokeza kwa upande wa vifaa vya mchezo huo nchini.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG