PICHA NA HABARI NA JOHN BANDA, DODOMA
Diwani wa
Kata ya Buigiri, Wilaya ya Chamwino, Mkoani Dodoma Mhe. Kenneth Yindi ametoa
wiki mbili kwa Kamati ya Maboresho ya Makazi ya Kijiji cha Buigiri iweze
kumpelekea taarifa juu ya matumizi ya fedha zaidi ya milioni 12 zilizochangwa
na Wananchi zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Akizungumza katika Mkutano Maalumu wa kusikiliza kero za
Wananchi juu ya mgogoro wa ardhi kati ya Kijiji cha Buigiri na Halmashauri ya
Wilaya ya Chamwino uliodumu kwa miaka tisa Mhe. Yindi amesema anahitaji kupata
ufafanuzi juu ya fedha hizo zilivytumika mpaka sasa ikiwa ni pamoja na kupata
stakabadhi za malipo mbalimbali yaliyofanywa kwa ajili mradi wa Maboresho ya
makaazi vinginevyo fedha hizo zirejeshwe na sheria ichukue mkondo wake
“haiwezekani wananchi wa wajibane kwa kuacha kufanya mambo
yao mengine ya kimaisha wanachanga pesa kwa kujinyima wakidhani zinawasaidi kwa
wakati lakini cha ajabu tangu wamechanga zaidi ya mwaka mmoja uliyopita mpaka sasa hakuna
matokeo yoyote yaliyo wazi na yenye tija kwa ajili ya makaazi yao
Sasa natoa wiki mbili mchanganuo wa matumizi pamoja na
stakabadhi za fedha za wananchi zaidi ya 12 mil tuwe tumeupata toka halmashari vinginevyo tuone hatua nyingine za kuchukua”, alisema
AIDHA Diwani huyo amesema kuwa imefika wakati wanachi wa
Buigiri waruhusiwe kufanya kazi na Makampuni yanayojihusisha na upimaji
Ardhi ambayo yanaweza kutumia muda mfupi
kuwapimia wananchi kama ilivyo kwa halmashauri nyingine ikiwemo halmashauri ya
jiji Dodoma ambalo kwa kiasi kikubwa imefanikiwa katika upimaji ikiwemo kuondoa
migogoro na wananchi kuhusu Ardhi
Kutokana na swala hilo kumgusa Afisa Ardhi na Maliasili
Halamshauri Wilaya ya Chamwino Rugambwa Banyikila ambaye Ofisi imekuwa ikifanya
kazi na Kamati ya Maboresho ya Makaazi amesema fedha hizo hazijapotea wala
kutumika vibaya hivyo yuko tayari kuonesha mchanagnuo wa matumizi yake pamoja
na stakabadhi zote kwani zipo kwenye faili la kumbukumbu za mradi husika.
Hata hivyo mgogoro huo ambao umedumu kwa takribani miaka tisa
umeonesha tumaini la kupata ufumbuzi baada ya Ofisi ya Mkurugenzi Wilaya ya
Chamwino kukubali mapendekezo kutoka kwa Wananchi wa Kijiji cha Buigiri
kutafuta Makampuni yatakayofanya kazi ya kupima Ardhi kwa kushirikiana na
Kamati Maalumu ya Wananchi, zoezi ambalo kwa mujibu wa Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya Athuman Masasi halitachukua zaidi ya Mwezi mmoja kutoka
leo mei 16,2018.
Tags
ARDHI





