BANDA MEDIA BLOG

No title

 TAASI YA UTAFITI WA KILIMO TANZANIA (TARI) YAJIDHATITI KUOKOA MABILION YANAYOPOTEA KILA MWAKA KUAGIZA MAFUTA YA KULA NJE

Mtafiti wa kilimo toka Idara ya usambazaji wa Teknolojia na uhusiano Hamis Amanje akionyesha mkungu wa mchikichi uliozalishwa na mbegu bora aina ya TENERA



mawese yanayozalishwa na mbegu aina ya TENERA

Na John Banda, Dodoma

KATIKA kuhakikisha kuwa kiasi cha fedha Zaidi ya bil. 3 zinazotumiwa na serikali kuagiza mafuta nje zinaokolewa Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) imebuni na kutengeneza mbegu ya mchikichi aina ya TENERA ambayo kwa sasa inazalisha mafuta kwa wingi tofaiti na awali

Kauli hiyo imetolewa na Mtafiti wa kilimo toka Idara ya usambazaji wa Teknolojia na uhusiano Hamis Amanje wakatai akiongea na waandishi wa habari katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma ambako taasisihiyo inashiriki maonyesho ya Ubunifu MAKISATU ambapo amesema hivi sasa uzalishaji wa mafuta aina ya mawese umeongezeka.

Amanje amesema mbegu ya TENERA ni bora kwa sababu miche yake inaanza kuzaa na kukomaa kati ya miaka 3 hadi mine toufauti na mbegu ya awali ambayo ilikuwa ikitumia miaka 5 hadi 6 huku mbegu zake zikitoa mafuta kidogo.

Amesema tangu mbegu hiyo ilipobuniwa na kuanza kutumika mwaka 2018 uzalishaji wake umeongezeka kwa kipindi cha miaka mitatu mpaka kufikia tani 4 mpaka 6 kwa hekta moja na kwamba mafuta ya kula nchini yanapatikana kwa Zaidi asilimia 60 na mapambano yanaendelea ili kufikia asilimia Zaidi ya 100.

                      mafuta bora ya mawese

Ameongeza kuwa usambazaji wa miche bora ya michikichiki unaendelea kwa kushirikiana na wadau kuzifikisha katika halmashauri za wilaya katika mikoa mbalimbali ambapo kwa sasa baadhi ya mikoa ikiwemo ya Tabora, Mbeya na Kigoma zimeshafika

“kwa sasa mapambano yanaendelea ili tuweze kutimiza malengo ya serikali ya kuzalisha mafuta ya kula hapahapa nchini kwa Zaidi ya asilimia 100 toka asilimia 60 mpaka 70 za sasa ambapo fedha  hizo bil 3.6 ambazo zimekuwa zikitumika kuagiza mafuta nje zifanye kazi nyingine za maendeleo ya wananchi”, amesema

Aidha amewataka watanzania wanaozalisha miche kutumia njia rahisi ya mapipa ambayo yanatunza joto kwa kuweka mavumbi ya mkaa, majani na aina nyingine ya takataka ili kuepuka hasara ya kununua mashine za uoteshaji ambazo zinapataika kwa garama kubwa

huu ni mkungu wa Mchikichi wa mbegu ya zamani ambayo huzaa mkungu mdogo unaotoa mafuta kidogo.

MAONYESHO YA WIKI YA KITAIFA YA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UBUNIFU (MAKISATU), 2022 INAONGOZWA NA KAULI MBIU ISEMAYO “UBUNIFU KWA MAENDELEO ENDELEVU”,

 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG