BANDA MEDIA BLOG

No title

 MKUU WA WILAYA YA DODOMA MJINI AWATAKA WANAMAZOEZI KUMWAGILIA MOYO KWA STEP ILI KUEPUKA VIFO NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

Jamila Awadh aliyeibuka mshindi na kupewa zawadi baada kukimbia km. Zaidi 1,678 kwa mwaka huu wa 2022
mkuu wa wilya ya Dodoma mjini Jabiri Shekimweri akizungumza baada ya kumaliza mazoezi hayo ya km 10 na wanajogging wa Ilazo, Dodoma Runners, Makao makuu Fitness Club na FFU

              wanamakao makuu wakishiriki mbio hizo za mazoezi

mkuu wa wilya ya Dodoma mjini Jabiri Shekimweri mwenye kapelo nyekundu akikimbia pamoja na wanajogging wa Ilazo, Dodoma Runners, Makao makuu Fitness Club na FFU kwenye mbio za km 10

mkuu wa wilya ya Dodoma mjini Jabiri Shekimweri mwenye kapelo nyekundu waliochuchumaa akiwa katika picha ya pamoja na wanajogging wa Ilazo, Dodoma Runners, Makao makuu Fitness Club na FFU katika ukumbi wa chimwaga 


           Kamishna wa jeshi la Polisi, Charles Mkumbo akizungumza jambo mara baada ya kumaliza mazoezi hayo

Mkuu wa Wilaya akiwapa zawadi ya pongezi watoto hawa walio chini ya mikao 10 kwa kumaliza km zote 10
Makamu Mwenyekiti wa Makao Makuu Fitness Club Ernest Moses akipokea zawadi ya ushiriki wa mbio hizo zilizoandaliwa na DODOMA RUNNERS, toka kwa Dc 


                   ........................................................................................  

                              NA JOHN BANDA, DODOMA

MKUU wa Wilaya ya Dodoma mjini, Jabiri Shekimweri amesema  Kuelekea mwisho wa mwaka watanzania watunze Afya zao kwa kuendelea kufanya mazoezi

Shekimweri ameyasema hayo wakati aliposhiriki na kumaliza mbio za km. 10 zilizoandaliwa na DODOMA RUNNERS

Dc amesema “ni vizuri wanamazoezi kujichunga hasa kipindi hiki tunapoelekea mwishoni mwa mwaka kwa kufanya mazoezi na kuepuka kumwagilia moyo kwa kupindukia, tusipitilize tukaja poteza maisha au tukapata ukimwi”, amesema

Kwa upande wake Kamishna wa jeshi la Polisi, Charles Mkumbo amesema mwishoni mwa mwaka huwa kuna mambo mengi yakiwemo ya kusafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine hivyo kila mtu ajichunge

Kamishna Mkumbo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Timu ya Polisi Tanzania inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC  Amesema “mwisho wa mwaka kuna mambo mengi hivyo unaposafiri hakikisha unakwenda kwa mwendo wakawaida na watahadhali unapokuwa njiani kisha kasalimie wazazi na wakati wa kurudi rudi salama ili tuukaribisha mwaka vizuri”, amesema

Aidha katika tukio hilo Jamila Awadh ameibuka mshindi na kupewa zawadi baada kukimbia km. Zaidi 1,678 kwa mwaka huu  wakati kwa upande wa wanaume aliyeibuka mshindi wa kwanza kwa kukimbia  KM.4,640 kwa mwaka huu wa 2022 ambaye ni sawa na kwenda Mkoani Dar es laaam mara 10 kwa mguu

Vilabu waalikwa vya Jogging ambavyo vimeshiriki Mbio hizo ni pamoja na Makao Mkuu Fitness Club, Ilazo Jogging, Kikosi cha Kutuliza Ghasia cha Ffu Dodoma na Waandaaji Dodoma Runners


Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG