BANDA MEDIA BLOG

No title

 MWANGA AWATAKA VIONGOZI WA CCM KATA NA MATAWI KUFANYA VIKAO VYA KIKANUNI, WENYEVITI WA MITAA NAO WATAKIWA KIJITATHINI








BANDA MEDIA ONE, DODOMA

JUMUIYA ya Wazazi ambayo ni Jumuiya mama ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Dodoma mjini imefanya ziara ya kutembelea Kata Mbalimbali za wilaya hiyo na kutoa maagizo kadhaa Kwa viongozi wa chama hicho..

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Stiven Mwanga akiongea hivi karibuni mara baada ya kumaliza kutembelea Ujenzi wa vyumba vya madarasa na maabara katika shule ya sekondari na Vyoo na ofisi katika shule ya msingi zote za Kata ya Iyunbu wilayani humo moja ya mambo aliyoyasisitiza ni pamoja na kufanyika Kwa vikao vya kikanuni.

Amesma vikao vya CCM vya Kata, Tawi na Mashina hufanyika kikanuni kila baada ya miezi mitatu, ambapo vikao vya dharula hufanyika Wakati wowote hivyo viongozi kukaa bila kufanya vikao ni Sawa na kuua Chama...

"mfano kata ya hapa Iyumbu hakuna kikao chochote kilichofanyika Tangu kumalizika Kwa uchaguzi katikati ya mwaka 2022, hapo kutakuwa na chama kweli, 

Ni vizuri muitishe Vikao mkutane na wanachama kuanzia mashinani na huko ndiko kwenye watu huko nawakikishia mtakutana na changamoto za wananchi na itakuwa rahisi kuzitatua kuliko kuacha kila Mtu anaugulia maumivu yake mwenyewe", amesema

Aidha amewanyooshea kidole wenyeviti wa mitaa ambao wanatokana na Chama hicho kuwa na wao wanatakiwa kuitisha vikao ili kuchukua changamoto za wananchi na kuzifanyia Kazi.

"Uongozi siyo utawara ni kuwatumikia wanachi ukiwaongoza kwa kuwaonyesha njia na ndiyo maana waliwaamini na kuwachagua, katika Hili ni vizuri pia kila mmoja ajitathini mwenyewe kama anatosha au laa ili asije akikapa Kazi kubwa chama kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, 

Unakuta mwenyekiti chama kinamuamini na kumpa nafasi lakini baada ya kuchaguliwa anaanza kukidharau anakosa kukiheshimu na hata wengine kukiwa na shuhuli za chama au vikao kama hivi hawaonekani, kama hapa iyumbu ambapo kwa mitaa yote minne hakuna hata mmoja aliyeshiriki hii si dalili nzuri", amesema

Kuhusu Changamoto zilizoibuliwa katika Kata hiyo ni pamoja na ukosefu wa kivuko katika korongo linalotenga mitaa ya Udom na Nyerere kuliko na shule za msingi na sekondari ambapo mvua zikinyesha mawasiliano hukatika kutokana na maji kutwama, Wanachi pamoja na kulipia Aridh Kwa muda mrefu bado hawajapatiwa Hati, fedha zaidi ya 600.Mil ambazo bado Kata haijalipwa na kampuni ya ujenzi wa Reli ya mwendokasi kutokana na kuchimba na kuchukua kifusi katika mlima uliyopo mtaa wa iyumbu, ukosefu wa maji katika sehemu ya mtaa wa mwinyi pamoja na kutopimiwa mashamba Yao, vijana wakata hiyo kutonufaika na ufundi au vibarua Kwa miradi mbalimbali ya ujenzi inayofanywa na taasisi  mbalimbali.

Huku wanaccm wakiwataka viongozi wa CCM kukieneza chama hicho bila kuangalia Ukubwa wa Ukoo, Familia, Umaarufu wala utajili Bali uangaliwe uwezo wa mtu katika kuwaongoza na kuwasaidia wananchi

Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kuibua na kutatua changamoto katika Kata hisika ambapo Mwenyekiti Mwanga  aliambatana na mjumbe kamati ya utekelezaji Raimond Magoda, Mjumbe Halimashauri ya Wilaya Samwel Kisaro na mjumbe wa kamati ya utekelezaji toka jumuiya ya wazazi kwenga UWT,Ashura Kimwaga

 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG