BANDA MEDIA BLOG

CHADEMA NI KAMA KITINDAMIMBA, NCHI HAIWEZI KUENDESHWA KWA KUWADEKEZA _ ASIA JUMA

 

Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Asia Juma akimlisha kipande cha Keki Mmoja wa watu wasioona ambao nao walipata fursa ya Kupata afunzo hayo ya Ujasiriamali


................................................................................
NA MWANDISHI WETU, DODOMA

MJUMBE wa Baraza Kuu la Taifa la chama cha Mapinduzi CCM Asia Juma amesema Chama cha CHADEMA ni sawa na Mtoto wa Mwisho ambaye huwa haaichi kualamika na kuanzisha visa na wakati mwingine mikasa ili mradi asikike na kusaidiwa.

Ameayasema hayo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Ujasiliamali yalitofanyika kwa wiki moja katika kata ya Nkuhungu jijini Dodoma yaliyowajumuisha wakazi zaidi ya 150 wa kata hiyo.

Asia aliwataka wahitimu wa mafunzo hayo kutojihusisha na Maandamano yaliyoitishwa na Chama cha CHADEMA badara yake wakatengeneze, Biskuti, Batiki, Keki, Clpis, Karanga za Kusaga na bidhaa nyingine nyingi walizofundishwa Wakauze ili kuendelea kulea familia zao

“chadema ni kama kitinda mimba, kitinda mimba mara zote huwa hajiamini katika familia ndiyo maana huwa haishi kijilalamisha hata kwa mambo yasiyo ya msingi, malengo yake huwa anahitaji kusaidiwa ni mtu kudeka tu,

Huwezi kuendesha Nchi kwa kumdekeza  kitinda mimba ambaye kazi yake ni kujidekeza kwenye miguu ya mama yake, we ona Miswada yote ambayo wadau mbalimbali mpaka CHADEMA wenyewe waliyachangia maoni, lakini kabla hayajafika popote, tayari wametoka na kuanza kujilalamisha na kuwashawishi Watanzania waingie Barabarani kwa ajili ya maandamno kwani walijibiwa kuwa maoni hayafanyiwi kazi? Alisema na kuhoji.

Asia ambaye Pia ni Mjumbe wa Baraza kuu la UWT Taifa na mjumbe wa mkutano mkuu wa Mkoa wa Dodoma kupitia Wazazi amesema pia Kwenye Maandano huwa hamna ustaarabu wowote mtu anweza kushiriki kisha akaumia ingekuwa bora waachiwe viongozi kina MBOWE wenyewe na familia zao wakaandamane.

Hivi karibuni chama cha CHADEMA kupitia mwenyekiti wake  Ffreeman Mbowe kilitangaza maandamano ya Amani Bila kikomo Nchi Nzima, hadi Pale, Serikali Itakapofanyia kazi Maoni na Mapendekezo ya Wadau kuhusu upatikanaji wa Katiba Mpya na Chaguzi huru na Haki, ambapo alisema maandamano hayo yanatarajiwa kuanza siku ya Jumatano ya Tarehe 24 mwezi huu. 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG