Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Joseph Mhagama, akiongea Na Vyombo vya Habari katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo januari 22,2024
...........................................................
Na John Banda, Dodoma
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Sheria na Katiba,
imesema Imeshangazwa na Chama kimoja kati ya vyama 13 Vilivyoshiriki katika
utoaji wa Maoni ya Miswada ya Sheria ya Uchaguzi uliofanyika hivi karibuni
jijini Dodoma kwa kutoka hadharani na kutangaza maandamano kwa ajili ya kile alichoita kutaka kudhoofisha mchakato unaoendelea.
Hivi karibuni chama cha CHADEMA
kupitia mwenyekiti wake Ffreeman Mbowe kilitangaza maandamano ya
Amani Bila kikomo Nchi Nzima, hadi Pale, Serikali Itakapofanyia kazi Maoni na
Mapendekezo ya Wadau kuhusu upatikanaji wa Katiba Mpya na Chaguzi huru na Haki,
ambapo alisema maandamano hayo yanatarajiwa kuanza siku ya Jumatano ya Tarehe
24 mwezi huu.
Akiongea na Waandishi ya Habari kando ya Kikao cha
Kamati hiyo kilichokuwa Kikiendelea Leo Januari 22,2024 Bungeni Dodoma,
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Joseph
Mhagama amesema alitegemea viongozi wakuu wa Chedema kwa kuwa walishawahi kuwa
wabunge na wanajua utaratibu wangewaelekeza wananchi kuhusu hatua muhimu
zinazoendelea baada ya maoni kutolewa.
Mhangama amesema kamati hiyo ilipokea maoni yote ya
wadaua na kutengenezea jedwari kisha wakayapeleka Serikalini..
“baada ya kamati yangu kuyapokea maoni ya wadau
imeshakaa na kuyachambua kisha imetengeneza jedwari na kulipeleka serikalini,
kinachosubiliwa kwa sasa ni serikali kuja kwenye kamati kwa ajili ya
majadiliano na makubaliano”, amesema
Ameongeza kuwa baada ya taratibu za kamati ya
kudumu ya Bunge na serikali kukamilika kisha kukawa na baadhi ya vifungu havijakaa
sawa serikali itatengeza Jedwari ambalo litapelekwa Bungeni kwa wawakilishi wa
wananchi nao watapitia na litajadili kifungu kwa kifungu kipi kipite kipi
kisipite.
Amesema Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe,
Katibu mkuu wa Chama hicho Tundu Lisu na Naibu Katibu Mkuu, John Mnyika wao wameshwahi kuwa Wabunge na
utaratibu huo wanaujua ila wanachokifanya kuitisha Maandamano hayo ni kutaka kuwavuruga watanzania na kulivuruga
Bunge lisitekeleze wajibu wake wa Kikatiba.
“kwa maana hiyo hawa wenzetu wanataka kudharau
maoni yote yaliyotolewa na wadau pamoja na watanzania wote kwa ujumla”, amesema
Mhe. Mhagama amebainisha kuwa katika siku 4 za
kusikiliza na kukusanya maoni ya Wadau na watanzania Kamati hiyo ilishuhudia
idadi kubwa ya Uwakilishi kutoka katika makundi mbalimbali yakiwemo Taasisi za
Dini, Taasisi za kiraia, Vyama vya Siasa na wananchi wa kawaida idadi ikiwa 1,707
ambayo ni kubwa kuwahi kutokea katika utoaji wa maoni hapa nchini.







