NA, JOHN BANDA, DODOMA
KATIBU Mkuu wa CHAMA cha Mapinduzi CCM Balozi Dkt,Emanuel Nchimbi amesema kuwa
kama Chama watakuwa mstari wa mbele kutaka maridhiano na Vyama pinzani huku
akiwataka wanaCCM kubishana na Vyama vya upinzani kwa hoja kwakujitofautisha
kutokana na ukongwe Wake.
Ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati alipokuwa akipokelewa
katika viwanya vya CCM, Makao Makuu jijini Dodoma.
Dkt, Nchimbi amesema kila mwana chama anatakiwa kujua umuhimu
wake ndani ya chama kuanzia ngazi za mashina hadi taifa.
" Tukumbuke kuwa chama ni wana chama na ndio maana kazi ya
kukitangaza ni ya wanachama wenyewe, "Amesema Dkt Nchimbi
" Niwaombe Sana waana CCM kakitangazeni chama kwa ni
hakuna mwenye uchungu na chama chake kama mwanachama mwenyewe chukueni dhima
hiyo Kutakana kukitangazani chama kwa hoja nasio kwa ushabiki kitofautisheni
chama kikongwe hivi vyama vinavyochipukia, "Amesema Dkt Nchimbi
Aidha amewataka wanachama wote kuanzia ngazi ya Shina
kuhakikisha wanakitetea na kukisemea Chama vizuri kutokana na mambo mazuri
yanayofanywa na chama hicho
Kwa upande Wake,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,ROSEMARY SENYAMULE
amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na uchapa kazi Wake huku
akishukuru kwa miradi ya kimkakati inayotekekezwa Dodoma ikiwemo ujenzi wa
Standard gauge.
Awali Aliekuwa Mbunge wa CHADEMA Viti maalum,Upendo
Peneza ambaye amehamia CCM amemsifia Rais Samia SULUHU Hassan kuwa ni
mwanamageuzi wa kweli katika kusimamamia haki na Demokrasia ya nchi huku
akiahidi kutoa ushirikiano kwa CHAMA katika kuleta maendeleo
Hata hivyo Pendeza Amesema ameamua kuhamia CCM, kutokana na Rais
Samia kuweka mazingira Mazuri kwa vyama vya Siasa, wadau na wananchi kwa ujumla
kuhusu kuweka mazingira ya Umoja wa kitaifa kwa kukubali kukaaa pamoja kwa
ajili ya Maridhiano.
Kada huyo Mpya wa CCM, aliyehama Chadema ambako aliwahi kuwa
Mbunge wa Viti Maalum na mwenzake aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa
Manyara, Benson Andrew pamoja na Onesmo Mbuya katibi wa CHADEMA wilayani
Morogoro...