BANDA MEDIA BLOG

TAFITI ZA KILIMO NA UCHUMI KUKAMILIKA MWISHONI MWA MWEZI HUU

                                          Rosemary Senyamule Rc Dodoma 

                                            
                                              NA JOHN BANDA, DODOMA

  UTAFITI wa Kilimo na Uchumi uliaonza kufanyika mwishoni mwa mwaka jana unatarajiwa kukamilishwa ndani ya miezi miwili Mkuu wa mkoa wa Dodoma akiwataka wananchi kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Akiongea  leo Januari 15,2024 ukumbi wa Ofisini yake na Waandishi wa Habari, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema Utafiti wa kilimo unaofanyika ni wa mwaka 2022/23 ambapo tafiti hizi zinaiwezesha nchi  kupata Takwimu Rasmi ambazo zitatumika katika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya kikanda na Kimataifa.

 "Utafiti huu utafanyika katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara kwa kipindi cha siku 60 na umeanza Tarehe 5 Novemba 2023. Utafiti huu ni muhimu sana kwa kuwa sekta ya kilimo inachangia wastani wa asilimia 26.2 ya pato la Taifa, inatoa ajira kwa karibu asilimia 65 ya watu wote nchini, inatuhakikishia usalama wa chakula na ina mchango mkubwa kwa maendeleo ya sekta nyingine hususani viwanda.

 "Utafiti huu wa kilimo mwaka 2023/24 utafanyika Tanzania nzima kwenye jumla ya maeneo 1,352. Kati ya maeneo hayo , 1,234 ni ya Tanzania Bara na maeneo 118 ni Zanzibar. Jumla ya kaya za Kilimo 16,224 zitahojiwa nchi nzima. Kati ya hizi 14,808 ni za Tanzania Bara na 1,416 ni za Zanzibar. Utafiti huu utafanyika katika ngazi ya Kaya na katika ngazi ya Taasisi. Katika Mkoa wetu maeneo yaliyochaguliwa kufanyika utafiti huu ni 61" Amesema  Senyamule

 Aidha, Senyamule ametoa rai  kwa wananchi kutoa ushirikiano pindi wanapohitajika kufanya hivyo kwani kadri wanaposhiriki katika tafiti hizi ndivyo Serikali inapogundua changamoto mbalimbali zinawakabili na hatimaye kuchukua hatua stahiki. Pia amesema kushiriki tafiti ni sehemu ya mchango katika kuleta maendeleo ya Mkoa wetu na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

 Tafiti hizi zinafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu sura 351 ambayo inaipa mamlaka ya Kisheria ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kufanya tafiti mbalimbali za Kitakwimu ili kuzalisha Takwimu kwa ajili ya kutumika katika kutunga na kuhuisha sera, kupanga mipango na ya maendeleo na kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake.

Kwa Upande wake Mratibu wa Sensa Mkoa wa Dodoma Idd Muruke amesema tafiti hizo hazikukamilika kwa wakati ndani ya siku 61 na hiyo  ni kutokana na uwepo wa sikuku zilizopita za mwisho wa mwaka. 

 

 


Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG