Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Mwalimu Vicent Kayombo akifafanua jambo wakati alipoongea na waandishi wa habari ofisini kwake.
............................................NA JOHN BANDA , DODOMA
ASILIMIA 88.88 ya
wanafunzi walioandikishwa kujiunga
Darasa la Kwanza katika shule za Serikali mkoani Dodoma mpaka kufikia
Januari 17, mwaka huu wameripotiwa kuanza masomo
Akiongea na Waandishi wa
Habari Ofisini kwake Afsa Elimu Mkoa wa Dodoma Mwlalimu Vicent Kayombo amesema Jumla ya wanafunzi 71,536 wamerioti shuleni
kati ya wanafunzi 80,482 walioandikishwa na kutakiwa kujiunga na shule ambapo amesema walioripoti ni sawa na asilimia 88.88.
Kayombo Amesema kwa
Upandewa wanafunzi waliojiunga na Kidato cha Kwanza wamefikia asilimia 57.31, kutoakana
na walioripoti kufikia 30,306 ikilinganishwa na idadi ya 52,880 ambao wamepangiwa kwenye shule serikali za mkoa wa
Dodoma.
Akiongelea wanafunzi
waliojiunga madarasa ya Awali Kayombo Amesema mpaka kufikia Januari 17, mwaka
huu waliokwisha Ripoti Shuleni ni 55.364 kati ya wanafunzi 65.471
walioandikishwa kujiunga na masomo katika mwaka huu mpya wa Elimu ambayo ni
sawa na Asilimia 84.56
AMBAO HAWAJAJIUNGA
Akizungumzia wanafunzi
ambao bado awajajiunga na masomo mpaka sasa Afisa Elimu Huyo amesema kumekuwa
juhudi kubwa za kuhamasisha wazazi ili wawepeleke shule watoto wao zinazofanywa
na Serikali ya Mkoa.
“Mkuu wa mkoa wa Dodoma
Rosemary Senyamule amekuwa akitoa
maelekezo kuwa wanafunzi wote walioandikishwa na waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza, wapelekwe
shule na wazazi wao kwa muda ulipangwa na kama hawana sare za shule wapewe madaftari
na kalamu wakaanze masomo, vifaa vingine vya shule vitawakuta masomoni”.
amesema
Sambamba na hayo Mwl.
Kayombo ametoa rai kwa wazazi na walezi
kuhakikisha watoto wao wana hudhuria shuleni kila siku tangu siku
anayoanza shule na kuendelea kusimamia mahudhurio na maendeleo ya watoto wao mashuleni.