Askofu Dkt. Cholongani akifafanua Jambo wakati alipokuwa akihubiri kwenye Ibada hiyo.
Mwanasiasa Mkongwe Dkt. John Malecela akizungumza wakati alipotoa Salamu za Pasaka katika Ibada hiyo
Ibada na maombezi yakiendelea
Sehemu ya Waumini wa kanisa hilo
kwa ya Uvuke ikitoa huduma katika ibada hiyo
Ibada ya Ushirika
Waumini wakiendelea na Ibada ya pasaka katika kanisa la Anglakana Jijini Dodoma
(PICHA ZOTE NA JOHN BANDA WA BANDA MEDIA ONE. COM)
.........................................................................
NA JOHN BANDA, DODOMA
MKUU wa Majeshi Nchini
Jenerali Jacob Mkunda, amesema nchi ipo salama kutokana na uongozi imara wa
Serikali iliyopo madarakani chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani.
Jenerali Mkunda ameyasema hayo
leo Machi 31,2024 kwenye ibada kuu ya
Pasaka iliyoandaliwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) ikifanyika Kitaifa
katika Kanisa kuu la Aglikana Tanzania, Jijini Dodoma.
“Nataka mtambue kwamba
serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mama Dkt, Samia Suluhu Hassan ipo
imara, na mimi kama mkuu wa majeshi ya Tanzania niwahakikishie kuwa nchi ipo
salama”,amesema
Mkunda ameongeza kuwa Pamoja na
usalama wa nchi uliyopo wananchi wahakikishe wanaidumisha amani iliyopo nchini,
kwani kuna baadhi ya mataifa ambayo hayawezi kusheherekea sikukuu kama hizi kutokana
na kukosekana kwa amani.
“Mwaka huu kuna uchaguzi wa
serikali za mitaa na mwaka ujao kuna uchaguzi mkuu, kama hakutakuwa na amani
chaguzi hizo hazitaweza kufanyika vizuri, tambueni kuwa amani ni chanzo cha
maendeleo ya nchi yoyote hivyo rai, yangu kwa waumini na watanzania wote
tuidumishe amani iliyopo”, amesema
Awali akihubiri katika Ibada
hiyo Askofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT)
Dkt. Dickson Chilongani amewataka waumini na wasio waumini wa kanisa hilo
kumtanguliza Mungu katika mambo yao Badala ya kumpa masharti.
“Wapo watu wanajitanguliza
wenyewe kuliko kumtanguliza Mungu, ukiwasikia hata kwenye maombi yao wakiomba
wanampangia Mungu masharti, eti awape Mke wa aina furani au gari aina Furani au
kitu chenye hadhi au thamani furani, hiyo ni kujitanguliza mwenyewe tuache ili
mapenzi ya yake yatimie”,
Aidha Dkt. Chilongani
amesisitiza kuwa Wanawake wathaminiwe na waaminiwe kama Yesu alivyowaamini na kuwathamini.
“Kubwa Zaidi Kumekuwepo Kundi
la wanaume ambao wamekuwa wakimzodoa Rais Samia kana kwamba kazi anazozifanya
kwa ajili ya Taifa hawazioni kwa sababu tu ni mwanamke, watu wa namna hii ni wabinafsi
ambao hawatufai katika jamii yetu”amesema
Amesema katikati ya Mwaka huu
kanisa hilo litakuwa na Sinodi ambapo viongozi wa kushika nafasi mbalimbali kanisani watachaguliwa, “niagize kuwe na usawa kusiwe na nafasi maalumu kwa wanaume, wote
wagombee kwani wote tupo sawa kama yesu alivyowatumia wanawake kwenda kuwaambia
wanafunzi wake kuhusu kufufuka kwake maana wao ndiyo walijitokeza kaburini
kabla ya wananume”, amesema
nae Mwanasiasa Mkongwe na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. John Samwel Malecela aliyeshiriki ibada hiyo ya Pasaka wakati akitoa salamu zake amesisitiza Msamaha kwa waumini na wanajamii kwa ujumla kwakuwataka kuondoa visasi na vinyongo mioyoni mwao ili kuruhusu Mungu afanye kazi yake.