Erdogan
Jumapili . Mach 31, 2024
1030 GMT ( saa saba unusu mchana)
Uchaguzi wa serikali za mitaa "utaashiria mwanzo wa enzi mpya katika nchi yetu," Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema baada ya kupiga kura yake mjini Istanbul pamoja na mke wake Emine Erdogan.
Erdogan ambaye taaluma yake ya kisiasa ilianza kama meya wa Istanbul mwaka 1994, pia alitaja uchaguzi wa mwaka jana wa bunge na urais ambao ulipigwa vita vikali na anatumai kuwa "hizi zitakuwa muhimu katika mwanzo wa enzi mpya, karne mpya katika nchi yetu."
Baada ya kupiga kura katika wilaya ya Uskudar ya jiji hilo, Erdogan alisisitiza umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi huo, akiwataka raia wote wanaostahili "kujitokeza na kufanya chaguo lao."
0500 GMT ( Saa mbili za asubuhi) — uchaguzi wa serikali za mitaa waanza Uturuki
Upigaji kura ulianza kote Uturuki siku ya Jumapili ili kuwachagua mameya wa jiji, mameya wa wilaya, na maafisa wengine wa eneo hilo ambao watahudumu kwa miaka mitano ijayo, ikiwa ni pamoja na katika miji yenye ushindani mkali ya Istanbul, Ankara, na Izmir.
Upigaji kura ulianza saa 7 asubuhi kwa saa za hapa nchini na utaendelea hadi saa kumi jioni katika majimbo 32 ya mashariki, na katika majimbo yaliyosalia, vituo vya kupigia kura vilifunguliwa saa 8 asubuhi na kufungwa saa 5 jioni.
Katika uchaguzi wa mitaa wa Machi 31, zaidi ya wapiga kura milioni 61 kote nchini wanastahili kupiga kura katika vituo zaidi ya 200,000 huku wagombea kutoka vyama 34 vya siasa wakishindana.
Vyama vikuu vinavyoshindana ni Chama tawala cha Haki na Maendeleo (AK), chama kikuu cha upinzani cha Republican People's Party (CHP), Nationalist Movement Party (MHP), Good (IYI) Party, na Peoples' Democratic Party (DEM Party) .
Wapiga kura wanaweza tu kuwapigia kura wagombeaji wa ofisi katika wilaya zao. Baadhi ya vijana milioni 1.32 watapiga kura kwa mara ya kwanza.
Karatasi ya kura ya Istanbul ina wagombea 49.
Zaidi ya masanduku 1,000 ya kupigia kura yataundwa kwa ajili ya wapiga kura ambao hawawezi kwenda kwenye uchaguzi kwa sababu ya ugonjwa au ulemavu.
Siku ya uchaguzi, uuzaji na unywaji wa aina zote za vileo vitapigwa marufuku kabisa katika maeneo yote yanayotoa pombe na kumbi za umma kuanzia saa 6 asubuhi hadi saa sita usiku wa manane.
Vituo vya redio na utangazaji haviruhusiwi kutoa habari, ubashiri au maoni kuhusu matokeo ya uchaguzi au uchaguzi hadi saa 12 jioni (1500 GMT).
Kuanzia saa 12 hadi saa 3 jioni (1500-1800 GMT), matangazo yanayohusiana na uchaguzi yanaweza tu kutumia habari na matangazo kutoka kwa Baraza Kuu la Uchaguzi (YSK).
