BANDA MEDIA BLOG

WANAWAKE ZAIDI YA MILIONI 6 HUPOTEZA MAISHA KILA MWAKA BARANI AFRICA KUTOKANA NA SARATANI YA MLANGO WA SHINGO YA KIZAZI

AFISA mipango wa Chanjo Taifa (MOH) Lotalis Gadau akielekeza jambo wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dodoma
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Kinga,Wizara ya Afya,Dk.Tumaini Haonga akizungumza jambo
Waandishi wa habari wakiwafuatilia matukio kwenye warsha hiyo


Waandish wa Habari jijini Dodoma wakifuatilia jambo wakati walipokuwa kwenye Warsha ya Saratani ya Mrango wa Shingo ya Kizazi iliyotolewa na Wizara ya Afya Kitengo cha Chanjo

                                                   ..............................................................

NA JOHN BANDA, DODOMA

AFISA mipango wa Chanjo Taifa (MOH) Lotalis Gadau amesema Takwimu zinaonesha kunakuwa na maambukizi mapya ya ugonjwa wa saratani ya Mlango wa Kizazi kwa wanawake zaidi ya Milioni 10, huku wanaopoteza maisha ni zaidi ya Milioni 6 Barani Afrika kwa kipindi hicho.

Afisa Mpango kutoka Wizara ya Afya akitoa mafunzo kwa waandishi wa Habari, kuhusu chanjo ya saratani ya mlango wa shingo ya kizazi (HPV) kuelekea maadhimisho ya Wiki ya chanjo ambayo itaanza Aprili 22 hadi 28 mwaka huu amesema Zaidi ya Watoto wenye umri kuanzia miaka 9 hadi 14 atapatiwa chanjo hiyo.

Kutokana na hilo Gadau amebainisha kuwa Tanzania ni nchi ya Tatu kwa kuwa na idadi kubwa ya Wagonjwa wa Saratani ya Mlango wa kizazi katika Bara la Afrika ikitanguliwa na Nchi Jirani ya Uganda

Pamoja na hayo amesema kuwa wagonjwa wengi takribani 70% wamekuwa wakifika katika Vituo vya Afya wakiwa na hali mbaya na kutoa wito kwa jamii kuhakikisha wanakuwa na utaratibu wakupima Mara kwa mara ili kuwa rahisi kupata matibabu iwapo kutakuwa na kubainika maambukizi.

Akielezea kuhusu Chanjo ya Saratani ya Mlango wa shingo ya kizazi amesema Chanjo hiyo ni salama na ni dozi ya Mara moja na inatolewa tofauti na awali ilikuwa inatolewa kwa awamu mbili ambapo wanaopatiwa chanjo hiyo ni watoto wakike kuanzia umri wa miaka 9 hadi 14.

Ni muhimu sasa kwa wazazi kuhakikisha wanawahamasiha Watoto wao kujitokeza kupata Chanjo hiyo ya HPV ili kuwalinda na maambukizi ya ugonjwa huo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Kinga,Wizara ya Afya,Dk.Tumaini Haonga amesema kutokana na ugonjwa kuwa na Kinga Serikali imeamua kuwe na Mpango wa kutoa Chanjo hiyo kwa Watoto na mabinti ili kupambana na ugonjwa huo.

Dkt. Haonga amesema baada ya utafiti na ufuatiliaji wa mara kwa mara unaofanywa na shirika la Afya Duniani (WHO) Pamoja na wadau wengine Imeinika chanjo ya Pili imekuwa ikiachwa kutokana na hapo awali kuwa wanapewa Watoto wenye umri wa miaka 14 ambao pia walikuwa wakimaliza darasa la 7.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG