BANDA MEDIA BLOG

JUMUYA YA WAZAZI WAMPA KONGOLE RAIS SAMIA KWA BAJETI 2024/25

 



NA JOHN BANDA, DODOMA

JUNE 13, siku ya Alhamis Mawaziri wa Fedha wa Nchi za Africa Mashariki Wamesoma Bajeti Kuu za Serikali zao kwa mwaka huu wa Fedha wa 2024/25 ambazo zinaingia kujadiliwa na Mabunge ya Nchizo ambapo kwa Tanzania Jumuiya ya wazazi ya Chama kinachoongoza Dola cha CCM kimetoa pongezi kwa makadilio hayo ya Bajeti yaliyosomwa na Waziri mwenye Dhamana hiyo Dk. Mwigulu Nchemba

 

Pongezi hizo zimetolewa mapema leo June 14,2024 na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM, Fadhari Rajabu Maganya wakati akiongea na Waandishi wa Vyombo mbalimbali vya Habari jijini Dodoma.

 Amesema kuwa bajeti imejaa matazamio mema ambayo yanabeba maisha ya wananchi wa Tanzania kwa kuboresha huduma mbalimbali Kama ambazo zilitajwa na Mhe.Waziri Nchemba.

"Sisi Jumuiya ya Wazazi Mimi kama kiongozi wake ninampa Mhe.Rais Kongole,Kongole hii ni kwa kuwa bajeti hii inabeba matumaini ya Watanzania, kwa hiyo tukaona kama Jumuiya tutoe kauli yetu ya kuipongeza Serikali kwa namna ambavyo imeendelea kuwajali watanzania na kuwapatia nafuu ya maisha kadri inavyowezekana"amesema 

Aidha amesema kuwa Tanzania si nchi iliyoendelea,Tanzania ni nchi inayoendelea kwa hiyo Maendeleo ni mchakato.

"Kwa hiyo tunaungana na Mhe.Rais na Serikali yake ya Chama Cha Mapinduzi ambayo anaiongoza kwa namna ambavyo anaguswa na maisha ya wananchi na kwa kweli sote ni mashahidi tunaona anavyojitahidi kuupiga mwingi kwa kushuhulikia miundombinu na kero mbalimbali za wananchi” amesema 

Aidha amesema kero ya kikokotoo imekuwa ikiimbwa sana kwa siku za hivi karibuni lakini Serikali imeliona hilo na kulipatia majibu kwa vitendo kwa kuongeza toka asilima 33 iliyokuwapo awali mpaka kufikia asilimia 40,

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi kwa bajeti ambayo imegusa maisha ya Wazanzibar na Watanzania kwa ujumala.

Hapo jana Juni 13,2024 Waziri wa Fedha Mhe.Dkt.Mwigulu Nchemba aliwasilisha Bungeni mapendekezo ya bajeti ya jumla ya Shilingi trilion 49.345.7 kwa mwaka 2024/2025,ambapo ni sawa na ongezeko la asilimia 11.2 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2023/2024 ya shilingi trilion 44.388.1

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG