BANDA MEDIA BLOG

SERIKALI YASISITIZA MITIHANI KWA WALIMU KABLA YA KUAJILIWA

                     

                        ........................

                  NA JON BANDA, DODOMA

TUME ya vyuo vikuu (TCU) imekutana jijini Dodoma kwa ajili ya kufanya mapitio na marejeo ya Mitaala Mipya Huku Mgeni Rasmi akiwa Profesa Adolf Mkenda Waziri katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambaye ameweka Msimamo wa Serikali kuwa Walimu Wapya watafanya Mitihani kabla ya Kuajiliwa.

Mkenda ameitoa Kauli Hiyo June 7,2024 kwa waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza kutoa hotuba ambayo alisema si ya kufungua wala kufunga mkutano huo uliowakutanisha, Makamu Wakuu wa Vyuo Vikuu  na Vyuo vya Kati, Wakuu wa Vyuo Vikuu vishiriki Manaibu Makamu Wakuu wa Vikuu upande wa taaluma na wadau wa mbalimbali wa elimu .

Profesa Mkenda amesisitiza kuwa katika kutekeleza mitaala mipya ya elimu, walimu wapya watafanya mtihani kabla ya kuajiriwa na kwamba watakaofanya vizuri ndio watakaopata nafasi.

Prof Mkenda amesema ni muhinu wanaojiriwa kwa sasa kama walimu watafanya mtihani kama Kada zingine wanavyofanya lengo likiwa ni kupata walimu bora Zaidi.

"Tukumbuke kauli ya Mheshimiwa Rais (Samia Suluhu Hassan) tukiwa Zanzibar alisema jamani tumefika mahali tuna walimu akitafuta kazi anasema mimi nimekosa kazi ila anaambiwa  hata ualimu umekosa? Sasa hivi tunaenda sehemu ambayo mwalimu unakuwa bora na kazi yetu kubwa sio kuangalia watu wangapi wameajiriwa kazi yetu ni watu wangu wamepata walimu gani bora wa kufundisha,"amesema Prof Mkenda.

Kuhusu walimu kuwa na leseni amesema : "Kwa Sasa naomba nisilizungumze hili utaratibu utakapokamilika litatangazwa,"

Aidha, amesema kwa mujibu wa sera ya elimu  wataendelea kuwaendeleza walimu waliopo makazini  kwa kutumia rasilimali zilizopo.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) Profesa Charles Kihampa  amesema lengo la kikao hicho ni kujadiliana kwa pamoja kuhusiana na utekelezaji wa mabadiliko ya mitaala ya elimu.

Amesema wanataka ifikapo mwaka 2025-2026 mitaala yote iwe imefanyiwa mabadiliko kwa kuzingatia maoni ya wadau.

 "Kuna haja ya kijipanga mapema ndio maana tumekutana hapa ili tuweze kujadiliana kwa mapana na kutoka na majibu sahihi kuhusiana na mitaala yetu,"amesema Prof Kihampa.






Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG