Mwenyekiti wa tume hii Oda Gasinzigwa alisema Tume
ilipokea wagombea tisa wa urais na baada ya kuwachuja, watatu walitimiza
vigezo.
Rais Paul Kagame, ambaye ni mwenyekiti wa chama
tawala cha Rwanda Patriotic Front (RPF Inkotanyi), Mwenyekiti wa Chama cha
Democratic Green Party of Rwanda, Frank Habineza na mgombea wa kujitegemea
Philippe Mpayimana ndio waliotimiza vigezo.
Wagombea ambao wanakiuka matakwa hayo ni Herman
Manirareba, Innocent Hakizimana, Fred Sekikubo Barafinda, Thomas Habimana,
Diane Rwigara, na Jean Mbanda.
Kwa mujibu wa sheria, wagombea ambao faili zao
hazijakamilika wanaweza kuwasilisha nyaraka zao ambazo hazijakamilika kabla ya
Juni 14, tarehe ambayo orodha ya mwisho itawekwa wazi, kwa mujibu wa NEC.
Paul Kagame
Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame, ambae anapeperusha
bendera ya Rwanda Patriotic Front (RPF-Inkotanyi) - chama tawala nchini humo -
aliwasilisha ombi lake Ijumaa, Mei 17.
Kagame amekuwa rais wa Rwanda tangu mwaka 2000.
Mnamo 2017, alichaguliwa tena kuwa rais baada ya
ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 98 ya jumla ya kura zilizopigwa.
Philippe Mpayimana
Mgombea huru wa urais Philippe Mpayimana, alisisitiza
haja ya maendeleo endelevu kwa Rwanda na watu wake.
Ni jaribio la Philippe Mpayimana la pili kwa nafasi ya urasi baada ya kugombea tena mwaka 2017/ Picha: Wengine
Hilo ni jaribio lake la pili kwa nafasi ya urasi
baada ya kugombea tena mwaka 2017 alipopata asilimia 0.72 ya kura zote katika
uchaguzi ambao Kagame alishinda.
Mpayimana sasa ni mtaalamu mkuu anayesimamia
ushirikishwaji wa jamii katika Wizara ya Umoja wa Kitaifa na Ushirikiano wa
Kiraia (MINUBUMWE), nafasi ambayo ameishikilia tangu Novemba 2021.
NEC itatangaza orodha ya muda ya wagombea kwenye
tovuti yake Juni 6, na orodha ya mwisho Juni 14.
Frank Habineza
Frank Habineza, mwenyekiti wa chama cha Democratic
Green Party of Rwanda, anajaribu kuwa mkuu wa nchi tena, baada ya kushindwa
katika uchaguzi wa urais wa 2017 ambapo alipata asilimia 0.45 ya kura zote.


