............ NA JOHN BANDA, DODOMA
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Nchini,imewashauri
Viongozi wa Siasa na Dini,kuielimisha Jamii juu ya umuhimu
wakutunza na kuheshimu utu wa binadamu.
Pia Tume hiyo imeisisitiza Serikali kuongeza idadi ya
Askari na bajeti ili kukabiliana na mauaji yanayotokea pamoja na kulitaka Jeshi
la Polisi kuongeza jitihada za kuzuia makosa yasitokee.
Akiongea Ofisini kwake, Jijini Dodoma mbele ya waandishi wa vyombo
mbalimbali vya Habari, Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu, amesema
viongozi hao wakatoa elimu hiyo itakayosaidia kuondoa matukio ya mauaji ambayo
yamekuwa yakitokea katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Jaji Mwaimu ametoa
mfano wa mauaji ya Mtoto mwenye Ualbino,
Asimwe Novart ambaye alichukuliwa nyumbani kwao Kamachumu Mkoani Kagera May 30,
2024 na baadae mwili wake kukutwa kwenye kalavati, June 17,2024 akiwa ameuawa
na kukatwa baadhi ya viungo vya mwili wake.
“viongozi wa kisiasa na dini mnaona vitendo vinayofanywa juu
ya watu wenye ulemavu wa Ngozi, kutokana na Imani za kishirikina ambazo
husababisha watu wasio na hatia kuuliwa kwa lengo la kutaka kutajirika kupitia
viungo vya watu hawa
watoe elimu ili jamii
ijue umuhimu wa kutunza na kuheshimu utu wa binadamu wenzao”,
amesema
ameongeza kuwa Serikali ione umuhimu wa kuweka nguvu katika
maeneo ya mipakani hasa mikoa ya kaskazini Magharibi ambako matukio kama hayo
yamekuwa yakijitokeza kwa madai hayo ya Imani za kishirikina “ati viungo vya albino
vinaweza kusababisha upatikanaji wa madini kwenye migodi na pia uongozi kwa
wagombea wa kisiasa
Napenda kutoa wito kwa Serikali yetu kuhakikisha
inaliongezea nguvu Jeshi la Polisi kwakuongeza idadi ya Askari ili waweze
kukidhi mahitaji Pamoja na kuongeza bajeti ya vifaa ambavyo ni vitendea kazi
ili waweze kufika kwa haraka pale matuko ya kihalifu yanapotokea”, amesema
Licha ya ,hayo Mwaimu amebainisha kuwaTume ya Haki za
Binadamu na utawala bora,imekuwa ikipokea malalamiko mengi kuhusu
migogoro ya Ardhi Nchini, ambapo Mkoa wa Dodoma ndio unaongoza na
changamoto kubwa ikiwa kutokuwepo kwa ushirikishwaji.

“Suala la mipango miji ni zuri katika uendelezaji wa miji
hasa pale watu wa ardhi wanapokuwa wanafanya upimai ni vyema wakakaa na
wananchi na kuwashirikisha ili kuondokana na migogoro hiyo”.
Katika hatua nyingine,amesema wamekuwa wakipokea
malalamiko ya watumishi wa Umma kulalamikia ucheleweshwaji wa mafao kwa
wastaafu,mapunjo ya mshahara pamoja na Kikokotoo.
Hivi karibuni matukio kadhaa ya mauaji yameripotiwa likiwemo
la wilayani chamwimo julai 7, 2024
majira ya saa 4:30 asubuhi huko kijiji cha mheme, mtoto Goodluck mathias mwenye umri wa miaka 5
alinyongwa na baba yake wa kambo, Steven Mabula mwenye umri wa miaka 44 ambapo
chanzo cha tukio hilo, Steven alirudi nyumbani na mke wake wakiwa wamelewa wakaanza
kugombana kisha mkewe kukimbilia kwa jirani kujificha na aliporudi akakuta
mtoto wake ameshanyongwa na baba huyo wa kufikia.
Siku chache Baadae Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma, Theopista Mallya alibainisha mbele ya waandishi
wa Habari kuwa ndani ya Wiki mbili tayari watu 5 walishauawa kutokana na visa
vinavyosababishwa na ulevi.
MWISHO