NA JOHN BANDA, DODOMA
KAMPUNI za Mabasi za SHABIBY LINE na SATCO zinazotoa huduma
za kusafirisha Abiria kwa njia ya Barabara zimekabidhiwa Tuzo ya mshindi wa
kwanza na ya pili baada ya kuibuka washindi katika utoaji wa Huduma hiyo kwa abiria hapa
nchini.
Tukio la kukabidhiwa tuzo hizo
limefanyika Agosti 26,2024 katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma, kwenye
Uzinduzi wa Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Kitaifa na Maadhimisho ya
Miaka 50 ya Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambapo Makamu wa Rais. Dkt.
Philip Mpango amekuwa Mgeni Rasmi.
Akiongea kwa Furaha baada ya Kupata Tuzo hiyo Brand Manager
wa Kampuni ya SHABIBY LINE Nicolaus Johachim amesema Siri iliyowafanya kuibuka washindi,
ni Kutoa huduma kwa kuzingatia viwango vya Ubora Pamoja na kuziishi sheria za
barabarani kwa ajili ya Usalama wa Abiria na wafanyakazi.
“kwa upande wetu shabiby line tuzo hii Pamoja na zingine tulizowahi kuzipata huwa tunazielekeza kwa Abiria na wateja wanaotumia huduma zetu, na kwamba tunawaahidi kuendelea kutoa huduma bora zenye viwango vya kitaifa na kimataifa ambazo zitaendelea kwavutia wateja wetu:, amesema
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
Mabasi ya SATCO iliyoibuka mshindi wa Pili, Rubaiye Mabighut amewashukuru wateja
wao kwa kuwawezesha kupata tuzo hiyo lakini pia LATRA ambao wametambua mchango
wao katika utoaji wa huduma ya usafirishaji katika jamii ya Watanzania kiasi
cha kuwapa Tuzo ya mshindi wa pili.
“hatuna mengi ya kuwaahidi wateja wetu kwani huduma bora
ni sifa yetu kubwa, ndiyo maana kwa kuzingatia usalama wa abiria tunazingatia
sheria za barabarani hivyo Mabasi ya Kampuni yetu ya SATCO kutokua katika kundi
la Ajali za Barabarani”, amesema na kuongeza

