/NA JOHN ISAREAL, NANE-NANE DODOMA
KWENYE Maonyesho ya Kilimo na Mifugo yanayofanyika
kitaifa katika viwanja vya Nane nane Kitaifa katika viwanja vya Nzuguni Dodoma
kuna Mengi ya Kujifunza kwa wakulima, wafugaji na wananchi wa kawaida, leo nimekutana
na Dume la Ng’ombe aina ya Borani lenye umri wa Miaka 4 huku likiwa limezalisha
zaidi ya majike 206.
Kwa Mujibu wa Afisa Mifugo wa Halmashauri ya wilaya
ya Singida, Adam Sungita akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule
amesema kuwa Ng’ombe huyo ana uzito wa Kg 915. Ambao ni saw ana ng’ombe wa
kawaida watatu mpaka wanne.
Amewezaje kuzalisha idadi kubwa ya majike kwa kiasi
hicho, Sungita anasema kutokana na Muonekano wake wa kuvuti, uwezo wa kupanda
majike, uzito na ukubwa wa umbo lake vimekuwa ni vivutio tosha kwa wafugaji
wilayani Singida na wale wa mikoa Jirani, ambapo wengi majike wanayofuga
yanapofikia joto la kupata Mimba huwapeleka kuwapandisha na hakikia nao
wamefaidika kuipata mbegu hiyo.
Afisa huyo anasema wafugaji wengine Bado
hawajachelewa maana Borani huyo ndiyo
kwanza anaingia kwenye Ushebabi wa Ujana hasa akiwa na nguvu za kutosha kupanda
majike, hivyo wafike tu wakamshuhudie kwenye mabanda ya Wizara ya Mifugo
yaliyopo nane nane, wakamuone lakini pia wakapate Elimu kuhusu faida ya kufuga
aina hiyo ya Ng’ombe ambaye ni wa nyama ambapo nyama yake inatajwa kuwa ni tamu
na lainiiiii.
Sangita anasema anajivuni kwenye wilaya hiyo
anayofanyia kazi wafugaji Zaidi ya 40 wamefaidika kwa kubadilisha Maisha
kutokana na ufugaji wa kisasa huku wakipiga hatua za kimaendeleo katika Maisha
yao na hata Borani huyo anafugwa na mtu binafsi wala si taasisi.
“Mhe. Mkuu wa Mkoa Ng’ombe huyo kwa sasa anauzwa 12
mil. Kwa mtu atakayemuhitaji”, amesema