BANDA MEDIA BLOG

UDOM YAWAITA WANAFUNZI WANAOTAKA KUJIUNGA NA MASOMO NGAZI YA DIPLOMA HADI PHD. 2024/25 KUPATA USHAURI KWENYE BANDA LA MAONYESHO NANE NANE DODOMA

 


                              ..........................

  NA JOHN ISRAEL, NANE – NANE DODOMA

IKIWA zimesalia Siku mbili ili Darisha la Usaili kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na Masomo ya vyuo vikuu mwaka 2024/25 kufungwa, Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Kimewaalika kufika kwenye Banda lao lililopo katika Viwanja vya maonyesho ya Wakulima na Wafugaji Nane-nane Jijini Dodoma ili kupata ushauri.

Akiongea na Waandishi wa Vyombo mbalimbali vya Habari katika banda hilo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Chuo hicho Rose Joseph, amesema Dirisha la Usaili lilifunguliwa Julai 15, na kwamba litafungwa Agosti 10, mwaka huu, hivyo kuwataka wanafunzi wanaotaka kujiunga na masomo katika chuo hicho kuchangamkia fursa ya maonyesho ya Nanenane kwa kufika katika Banda lao ili kupewa ushari kabla ya kufanyiwa usaili.

Amesema wanafunzi wanapewa ushauri wa kozi za kusoma UDOM, kutokana na Ufaulu walio nao.

“tunawahamasisha watanzania wanaotaka kuja kujiunga na masomo katika chuo cha UDOM, kuja kwenye Banda letu ili wapewe ushauri wa kitaalam wa kozi za kuchukua kutokana na ufaulu walio nao, katika ngazi za kuanzia stashahada hadi shahada za uzamimu”, amesema na kuongeza. 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG