BANDA MEDIA BLOG

SWISSPORT YAJINADI NANE NANE DODOMA

 

Mmmliki wa kampuni ya Ufugaji, Ukusanyaji na  usambazaji wa maziwa ya ASAS, Fuad Asas akifafanua jambo wakaati alipokuwa akiongea na Organstus Hatiro,Denis Ngaila na Goodruck Walter ambao ni Waratibu wa Usafirishaji wa Mizigo wa Kampuni ya SWISSPORT, katika viwanja vya nanenane jijini Dodoma leo Agosti 8,2024

NA JOHN ISAREAL, NANE-NANE DODOMA

KAMPUNI ya Swissport pl Tanzania inayotoa huduma za Kupokea, Kuhifadhi na kusafirisha Mizigo nje ya nchi imewahamasisha wakulima na wote wenye nia ya kusafirisha mizigo nje ya nchi kufanya hivyo kwani Garama ni nafuu tofauti na uelewa wa watu wengi.

Mratibu wa Shughuli za  Usafirishaji Mizigo Nje ya Nchi, Denis Ngaila amemwambia Mwandishi wa Habari hizi, kwenye Maonyesho ya Kilimo na Mifugo yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni jijini Dodoma kuwa wapo watu wanaodhani masharti ni magumu au garama ni kubwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Metl, Indrabhuwan Singh akifafanua jambo wakaati alipokuwa akiongea na Organstus Hatiro,Denis Ngaila ambao ni Waratibu wa Usafirishaji wa Mizigo wa Kampuni ya SWISSPORT, katika viwanja vya nanenane jijini Dodoma leo Agosti 8,2024

Ngaila amesema Kampuni hiyo inasafirisha Matunda, Nyama, Maua na hata mizigo mingine kuwa watu wenye nia ya kutaka kuhudumiwa wafike katika viwanja hivyo vya nanane lakini pia kwenye ofisi zao zilizopo kwenye viwanja vya ndege vya Mwalimu Julius Nyerere na Kilimanajoro KIA.

Hata hivyo Mratibu huyo amesema wametoa na wanaendelea kutoa Elimu ya kutosha katika maonyesho hayo na kwamba mwitikio ni Mkubwa kwa wakulima hasa wa Parachichi. ambao wamekuwa wakisafirisha zao hilo kwa wingi kwenda nchi za bara Ulaya, Asia na kwa africa ni Afrika Kusini na Kenya.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG