BANDA MEDIA BLOG

TAPIFA YAIOMBA SERIKALI KUANZISHA BBT YA NGURUWE

NA JOHN ISAREAL, NANE-NANE DODOMA

SERIKALI imeombwa kutupia jicho Sekta ya Ufugaji wa Nguruwe kwa kuanzisha BBT ya mnyama huyo ambaye anatajwa kuwa na nyama pendwa Duniani kote.

Akioangea na waandishi wa Habari Katika viwanja vya Nane- nane jijini Dodoma Mwenyekiti wa Chama cha wafugaji wa Nguruwe hapa nchini (TAPIFA), Doreen Maro amesema imefika wakati ambao serikali inatakiwa kuitupia jicho sekta hiyo ambayo inaweza kuwatoa vijana haraka kwenye harakati za kiuchumi.

Bi. Doreen anasema kutokana na Ufugaji Bora wa Nguruwe  mnnyama huyo anaweza kuzaa mpaka mara Tatu kwa Mwaka ambapo kwa Uzao Mmoja huzaa kati ya  vitoto 15 hadi 20 ambapo kwa kipindi cha Miezi 6 nguruwe hufikisha uzito wa Zaidi ya Kilo 120.

“ufugaji wa kisasa wa nguruwe unalipa kwani kwa mwaka nguruwe mmoja anazaa vitoto kati ya 30 mpaka 60 kwa kuzaa mara tatu na ndani ya miezi 6 nguruwe hufikisha kilo 120 ambayo ni biashara inayolipa sana”, amesema

Aidha amesema Sekta hiyo ya ufugaji wa Nguruwe inatoa ajira kwa wingi hivyo Serikali inatakiwa itengeneze mazingira rahisi kwa wafugaji wachanga hata kwa kupitia mpango wa BBT kama ilivyo kwenye mifugo mingine.  

Amesema Mbegu bora ya nguruwe inayotoka nje ya nchi inapatikana kwa garama ya kati ya 500,000 na 600,000 hivyo kwa mfugaji mdogo si rahisi kumudu hivyo kama serikali ikitia mkono itawafanya wengi wanaotamani kujiunga na ufugaji wa mnyama huyo mwenye nyama pendwa Duniani kote.

Pia amewakaribisha wakazi wa Dodoma na mikoa Jirani wanaotembelea katika Viwanja vya Nane- nane wafike katika mabanda ya Mifugo husan kwenye ufugaji wa Nguruwe ili wakajipatie elimu ya ufugaji bora wenye tija.

Mnufaika ambaye ni mmiliki wa Shamba la Mbegu za Nguruwe la Marangu, Julieth Tarimo amesema katika ufugaji wanazingatia ubora ndiyo maana hata radha ya Nyama ya mnyama wanaefuga wao ni tofauti kwani haina mafuta, wala Shombo

“nguruwe wetu wanalala sehemu nzuri, wanakula chakura chenye ubora ambacho siyo makombo,wanakunywa maji ya bomba, niseme tu tunazingatia ubora katika ufugaji ndiyo maana nyama yake haiana shombo, mafuta wala haikinaishi”, amesema

Amewataka pia vijana wachangamkie kila fursa wanayoipata badala ya kusubiri ajira pekee.   











Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG