NA JOHN BANDA, NANE-NANE DODOMA
WANANCHI waliotembea Maonyesho ya Kilimo na Mifugo yaliyofanyika Kitaifa katika viwanja vya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma Wamekoshwa na Bidhaa Mpya zilizoonyeshwa na Kampuni ya KINGLION
Meneja Mauzo wa kampuni hiyo inayotengeneza na Kusambaza Pikipiki, Mabati na Maguta ya kubebea mizigo, Joseph Banzi akiongea kwenye banda lao la maonyesho nanenane amesema wananchi hao wamevutiwa na Bidhaa walizoonyesha.
Amesema Kampuni hiyo pia imetambulisha Bidhaa Mpya ya Water Pump na Jenereta Pamoja na Pikipiki mpya Kinglion 110 ambayo inatumia lita moja ya mafuta kwa umbali wa km. 70 ambayo tenk lake lina ujazo wa lita 13 kwa wakati mmoja.
hata hivyo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akihitimisha sherehe hizo za nanenane alitangaza kuwaongezea Wananchi siku mbali zaidi ambapo maonyesho hayo yatahitimishwa agosti 10 siku ya jumamosi na kwamba huduma zote zitaendelea kutolewa kama kawaida.