BANDA MEDIA BLOG

WAMILIKI WA DAYCARE ZINGATIENI USALAMA WA WATOTO - SHEKIMWERI

 

NA JOHN BANDA, DODOMA

MKUU wa wilaya ya Dodoma mjini Jabir Shekimweri amewataka wamiliki wa Shule za kulelea Watoto (DAYCARE CENTRE’S) kutimiza vigezo vilivyomo kweye usajili ikiwemo kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya usalama wa watoto.

Pia wahakikishe wanafanya kazi zao kwa kushirikiana na serikali badala ya kuwafanya baadhi ya Maafisa maendeleo ya jamii kuwa maadui.

Shekimweri ameyasema hayo wakati akiongea na wamiliki, walezi na walimu wa shule za awali waliokutana kwenye hafla ya kufahamiana na kubadilishana uzoefu Pamoja na kuzijadili changamoto zinazowakabili

Amesema jambo la msingi kwa wamiliki ambao bado hawana usajili ni kusajili vituo vyao, ambapo  ili kupata usajili huo lazima wapite na kupata utambulisho toka kwa viongozi wa serikali za mitaa wanakofanyia kazi.

Kabla ya kukaguliwa hakikisheni mnaweka mazingira mazuri kwa ajili ya usalama wa watoto

“Vituo hivi vipo kwenye mitaa, hakikisheni mazingira yake yanakuwa katika hali ya usafi ili kuepuka magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine, lakini pia usalama wa Watoto na walezi wao kutokana na vibaka”, amesema

Aidha Shekimwel amesema ili kufanya urahisi wa utendaji wa kazi wahakikishe wanafanya kazi karibu na serikali.

“kuna baadhi ya wamiliki ambao wamekuwa wakiwachukulia maafisa maendeleo ya jamii kama maadui wasiowatakia mema katika kazi zao lakini niwaambie tu hao walisomea fani ya malezi ya Watoto na wanapokuja kuwakagua msidhani ni wao bali taratibu za serikali mkitmiza vigezo haita wasumbua”, amesema

  

Awali Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wamiliki wa Vituo vya Kulelea Watoto (DAYCARE CENTRE’S) Dodoma, Rehema Mdengede amesema wamekutana katika khafla hiyo kwa ajili ya kufahamiana, kuzijadili changamoto zinazowakabili, Pamoja na kubadlishana uzoefu katika utendaji wao wa kazi, ambapo wadau mbalimbali wameshiriki Pamoja na serikali.






Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG