Askofu wa Kanisa Angalikana Tanzania, Dayosisi ya Biharamulo mkoani Kagera, Vithalis Yusuph Akifafanua jambo wakati alipokuwa akifungua Warsha ya CCMP Kwa watumishi wa kanisa hilo.
.........................
NA JOHN BANDA, BIHARAMULO
VIONGOZI wa dini Pamoja na Waumini wao wametakiwa kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha kwa
kujiwekea Akiba badala ya kutumia mpaka senti ya mwisho hali inayowasababishia
kutaabika pindi inapotokea dharula ya ugonjwa au Misiba kwa wapendwa wao
Ushauri huo Umetolewa na Askofu wa Kanisa Angalikana
Tanzania, Dayosisi ya Biharamulo mkoani Kagera, Vithalis Yusuph kwenye Ufunguzi
wa Warsha ya siku 5 kwa watumishi wa kada mbalimbali wa kanisa hilo inayolenga
kuzitambua Rasirimali na Fursa za kiuchumi ikiwa ni Pamoja na jinsi ya
kuzitumia (CCMP).
Askofu Yusuph amesema sababu kubwa inayowasababisha
baadhi ya Watumishi, Wakirsto na wanajamii kushindwa hata kusafiri kwa wakati
pindi inapotokea Msiba au Ugonjwa kwa wapendwa wao, ni kutokana na wengi wao
kushindwa kujiwekea akiba kupitia vipato wanavyovipata.
Amesema Baadhi ya Viongozi wa kanisa, wakristo na
wanajamii hushindwa kujiwekea akiba wakidhani ni lazima wawe na maburungutu ya
fedha ‘hapana’ “kwa mfano mimi wakati Fulani nilipokuwa nasoma nilikuwa najiunga
kwenye foreni benki nikiwa na Elfu 5 au 3 kujiwekea akiba, wakati wengine
wakiwa na mifuko iliyojaa noti lakini sikujali nilijua ninachokifanya
ninachokifanya ni kwa ajili ya baadae yangu.
“kujiwekea akiba si kutokana na ukubwa wa kipatao
unachopata bali ni utashi”, amesema
Akizungumzia Mafunzo ya CCMP, Askofu huyo amewataka
wachungaji kwenda kuwasaidia watu li waondokane na Umasikini kwa kuwafundisha
jinsi ya Kuzitambua Rasirimali na Frusa walizonazo kwenye mazingara yao na kuzitumia,
akitoa mfano wa matikiti ambayo maiaka ya nyuma yalitumika kuwapa Ng’ombe na
mifugo mingine kipindi cha uhaba wa maji, bila kujua hiyo ni rasirimali ya
kiuchumi.
Ameongeza pia kwa watumishi waaonafanya kazi na
kupata Mshahara ni vizuri waigeuze kuwa Rasirimali ya kuanzisha Miradi ya
kiuchumi badala ya kuitumia yote huku wakiwa na matumaini ya kupokea tena
mwisho wa mwezi ujao.
“hakuna mtu anayeweza kuwa Tajiri au kuwa na uchumi
mzuri kupitia msahara anaoupata mwisho wa mwezi, geuzeni fedha manazopata
kwenye mishara kuwa fursa za kujiendeleza kiuchumi badala ya kuzitumbua zote
huku mkisubiri kupokea mwezi mwingine”, amesema
Kwa Upande wake Mkuu wa Chuo cha Biblia Mkoani
Morogoro, Kasisi Samweli Maduma amesema Mungu alipomuumba Mwanadamu na kumuweka
kwenye Dunia yenye kila Rasilimali alitaka aishi Maisha ya Utosherevu
“kwenye Bustani ya Edeni kulikuwa na ardhi, mito,
miche izaayo matunda na madini ya aina mbalimbali hizo zote ni rasilimali za
kumfanya mtu aishi Maisha ya utosherevu kubwa ni kuzitambua na kisha kufanyia
kazi ili tuweze kuyafikia maendeleo ya kiuchumi”, amesema
Kasisi Zacharia Samson wa Dinari ya Chato amesema
Umasikini ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya kihuduma ambapo amesema mafunzo
hayo ya CCMP yamekuja kwa wakati muafaka ambao kanisa na jamii linayahitaji.
Mratibu wa Ushirika wa Wamama wa Kikristo wa
Anglikana Tanzania Kanda ya Ziwa Judith Kaigarula amesema ni vizuri waliopata
mafunzo hayo kwenda kuyafanyia kazi ili watu wazijue Rasilimali na fursa za
kiuchumi ili wakazifanyie kazi kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi.
“umasikini unachangia kwa kiwango kikubwa hata kazi ya Mungu kutofanyika vizuri kutokana na wakristo kushindwa kuwa na fedha hata kutoa sadaka kwenye ibada”, amesema