
Mashambulizi ya kijeshi ya Israel katika Ukanda wa Gaza yamesababisha vifo vya takriban watu 70 katika siku ya mwisho, matabibu wa Palestina walisema Jumamosi, wakati wapatanishi wakizindua msukumo mpya wa kusitisha mapigano ili kumaliza vita vilivyodumu kwa miezi 15.
Takriban watu 17 kati ya waliofariki waliuawa katika mashambulizi ya anga dhidi ya nyumba mbili katika Jiji la Gaza, la kwanza likiwa limeharibu nyumba ya familia ya Al-Ghoula saa za mapema, madaktari na wakaazi walisema.
"Mnamo saa 2 asubuhi tuliamshwa na sauti ya mlipuko mkubwa," alisema Ahmed Ayyan, jirani, na kuongeza kuwa watu 14 au 15 walikuwa wakiishi ndani ya nyumba hiyo.
Wengi wao ni wanawake na watoto, wote ni raia, hakuna mtu aliyerusha makombora, au kutoka kwa upinzani," Ayyan aliambia shirika la habari la Reuters.
Watu walitafuta vifusi kwa ajili ya manusura walionaswa chini ya vifusi hivyo na walisema watoto kadhaa walikuwa miongoni mwa waliouawa.
Jeshi la Israel limesema wale wote "waliolengwa katika shambulio hilo walihusika katika shughuli za kigaidi, ambazo ni pamoja na kutumia njia za misaada ya kibinadamu" na kwamba shambulio hilo lilifanyika mbali na "malori ya misaada na halikuathiri kuendelea kuingia kwa misaada ya kibinadamu."