Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo pamoja na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba waliwasilisha Mapendekezo ya Serikali ya Mpango, Kiwango na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Vile vile, Mkutano huo ulihudhuriwa na Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu na Katibu wa Bunge, Ndg. Baraka Leonard.







