BANDA MEDIA BLOG

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI SASA KUKUTANA NA STELLENBOSCH YA AFRICA YA KUSINI

 


Ushindi huo ulifanya matokeo ya jumla kuwa sare ya 2-2 kufuatia Al Masry kushinda 2-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa April 2 mjini Ismailia.

Kipa wa Simba SC Mguinea, Moussa Camara ameibuka shujaa kwa kuokoa mikwaju miwili ya penalti za viungo Mohamed Gaber Tawfik Hussein na Mahmoud Hamada Awad, huku Fakhreddine Ben Youssef akimfunga bao pekee.

Waliofunga penalti kwa Simba SC ni Ahoua, Mukwala, kiungo mshambuliaji Kibu Denis Prosper, Beki Shomari Salum Kapombe.

Simba SC sasa itakutana na mshindi wa jumla kati ya wenyeji Zamalek na Stellenbosch ya Afrika Kusini zinazorudiana usiku wa leo Uwanja wa Cairo International baada ya timu hizo kutoka suruhu kwenye mchezo wa kwanza April 2, katika Uwanja wa DHL Cape Town.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG